October 2 1980, Muhammad Alli anachakazwa vibaya sana na Larry Holmes. Kabla ya pambano madaktari walimkataza Alli kupanda ulingoni kutokana na hali mbaya ya afya yake. Ila walisahau huyu ni Muhammad Alli, binadamu asiyeamini katika kushindwa na kupoteza. Alilazimisha kupigana akiwa mgonjwa akaambulia kipigo cha ‘mbwa mwizi’
Jukwaani alikuwepo mshikaji wa karibu wa Alli, Cus D’Amato aliyekuja na mvulana mdogo wa miaka 14, Alimuokota katikati ya mji akiwanyang’anya watoto wa kizungu chakula na kuwapiga vibaya. Huyu mtoto aliiabudu mikono ya Muhammad Alli, Aliyahusudu maisha yake na kuuishi unyama wake. Huyu mtoto wa kuitwa Mike Tyson.
Mike Tyson alirudi nyumbani hawezi kuongea, hawezi kula wala kulala. Ilibidi Cus ampigie Alli simu na kumuambia “nipo na kijana fulani hapa, ana ndoto za kuwa Muhammad Alli, tafadhali ongea nae”. Tyson alishika simu na kuzungumza sentensi moja tu, “Jana nimekutazama ‘live’ kwa mara ya kwanza, usihofu nitakulipia kisasi siku moja.” Ikaisha hivo.
Muda haugandi na jua halikawii kuchwa, Larry Holmes alistaafu ngumi na kurudi nyumbani kupumzika. Tyson alikuja kuitikisa dunia. Holmes akiwa na miaka 38 alitamanishwa kurudi ulingoni kupambana na Tyson kwa kitita cha dola 3 milioni. Tyson alikuwa tayari kupambana bure, pesa si kitu mbele ya kisasi alichokifuga kwa zaidi ya miaka nane.
Pambano likaandaliwa na kupewa jina la ‘Heavy weight history’. Saa hiyo dunia inakumbuka kuwa Holmes hajawahi kupigwa kwa ‘KO’. Muhammad Alli alialikwa kama mgeni wa mpambano. Kabla ya kengele kulia alimfuata Tyson na kumnong’oneza “kumbuka ulichowahi kuniahidi, wakati ni sasa”. Tyson hakumuangusha, ndani ya raundi nne tu Holmes alikula KO ya kwanza ya maisha yake.
Historia yake inaanzia ndani ya jela ya watoto mjini New York akiwa na miaka 13. Hii ilikuwa mara ya 38 analetwa ndani kwa makosa tofauti. Maafande hapa walimshazoea, ilifika muda wakampa sero yake binafsi yenye jina lake. Alishazoea kuletwa hapa. Si Mapadre wa Roma wala Masheikh wa Saudia waliodhani kama Tyson anaweza kubadilisha tabia
ITAENDELEA..
Ondoka na Mkwanja Kwenye Tsh. 160,000,000
Hii ndiyo burudani yenye ushindi! Ingia kwenye kasino ya Meridianbet kufukuzia ushindi huu.
Flomena
Good news
Sabrina
Duuh mohamedi Ali alikua gwiji
Amiri Kayera
Huyu ndo Mike Tyson
Isha
Noma sana Tyson
Issa
Mike tyson ngumi jiwe
Dorophina
Tyson ni mwana ndondi mahiri sana
magdalena
tyson katika dimba la ngumi yupo makini sana na anahakikisha anapata ubingwa
Angelina
Goodupdate
Zeiyana
Tyson history yake haiwezi kufutika
Caroline
Nasubiria muendelezo jmn
Lydia Emmanuel Magoti
Huyo ndio Tyson alikuwa anaga kazi mbovu ana history nyingi yakimabavu
Tatu
Kumbe Muhammad ally ndiye aliyemtoa tyson
warda
Habari nzuri sana
Salma ngende
Habari nzuri
Shani
Iron tyson alikua balaa na uwezo wake mkubwa ulimwengun
Elika
Tyson ni mwana ndondi yuko vizur sana
Khadija
Habari njema sana
Fatuma kasomo
Tayson yuko vizuri
Hopemwaikuka
Tyson mnyama
Gabriel
Iron tyson alikua balaa
Janeflora malisa
Saf
Adelta
Tyson Ni mwenye history ktk ulimwengu wa ndondi
Povel
Mike TYSON ( iron MAN) mambo ni moto
Saupha mohamed
Mike Tyson MTU mbayaw
felister
duh nasubiria mwendelezo
Sauda
Tyson noma
Mwajumah
Noma sana Tyson
Ernest
Tyson mzee wa ngumi jiwe