Kell Brook Atundika Glavu Akiwa na Miaka 36

Bondia wa Uingereza Kell Brook ametangaza kustaafu mchezo wa ndondi akiwa na umri wa miaka 36.

Uamuzi huo wa kustaafu umekuja miezi mitatu baada ya kumchapa Amir Khan katika raundi 6 huko Manchester mwaka huu mwezi wa pili.

Bingwa huyo wa ubingwa wa dunia wa IBF welterweight alikuwa na uwezekano wa kuchapana na Chris Eubank Jr na Conor Benn lakini sasa bondia huyo ameamua kutundika glovu akiwa na rekodi ya kushinda mapambano 40-3.

Vipigo vitatu vya Brook kilikuja dhidi ya majina mashuhuri kama Gennady Golovkin, Errol Spence Jr na Terence Crawford.

Akizungumza na Sunday Telegraph, alisema: “Nimekuwa na mazungumzo ya muda mrefu na familia yangu na wazazi wangu, na yamepita kwangu. Sitapigana tena.

“Ni hisia kidogo kusema hivi kwa sauti kubwa. Mama yangu amefarijika. Nadhani kila mtu karibu nami amefurahishwa.

“Ndondi ni mchezo mgumu na hatari sana na unaweza kupoteza maisha na sasa nimemaliza nikiwa na uwezo wangu wote.”


TENGENEZA FAIDA NA ZEUS ANCIENT FORTUNES

Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe