Kehl: Sitashangaa Haaland Akisonga Mbele

Erling Haaland ataweka mambo wazi juu ya mustakabali wake wiki ijayo, kulingana na mkurugenzi wa michezo wa Borussia Dortmund Sebastian Kehl, ambaye amekiri kwamba hatashangaa kama fowadi huyo ataondoka msimu huu wa joto.

Kehl: Sitashangaa Haaland Akisonga Mbele

Manchester City wanatajwa kuwa mstari wa mbele kuwania saini ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Norway, ambaye alijiunga na Dortmund mwishoni mwa Disemba 2019 baada akitokea Salzburg.

Kehl aliliambia shirika la utangazaji la Ujerumani Sport1: “Nadhani tutakuwa na uwazi wiki ijayo. Sitashangaa kama angesonga mbele mwishowe.”

Miamba wa Uhispania Real Madrid na Barcelona pia wamekuwa wakihusishwa sana na Haaland, lakini matarajio ya kuhamia LaLiga yameonekana kupoa katika miezi ya hivi karibuni.

Baba wa Haaland, Alf-Inge, alikuwa akichezea City na mshambuliaji wa Dortmund alizaliwa Leeds, kwa hivyo kuhamia England kunaweza kutarajiwa.


TENGENEZA FAIDA NA ZEUS ANCIENT FORTUNES

Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe