Bayern Munich walijitupa uwanjani siku ya Jumatano kuendelea na mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya ambapo walikuwa ugenini katika dimba la Estadio da Luiz kuumana na Benfica na timu zote zilichezwa vyema katika kipindi cha kwanza hali iliyopelekea kwenda mapumziko kwa bila kufungana.

Magolikipa wa timu zote walikuwa imara langoni kuhakikisha hakuna mpira unaingia lakini dakika 20 za mwisho Bayern walimaliza mchezo kwa mtindo wa aina yake na kuibuka na ushindi wa 4-0.
Leroy Sane ndiyo alieanza kuilegeza ngome ya Benfica kwa kufunga bao baada ya kupiga free kick safi dakika ya 70 dakika 10 baadaye Everton Soares alijifunga akijaribu kuepusha mpira wa hatari njaa ya Bayern iliendelea kuonekana kwani dakika ya 82 Robert Lewandowski alifunga bao la tatu na 16 kwa msimu huu katika michezo 12.

Kingsley Coman alikuwa ni injini ya mambo yote kutokea akionyesha kiwango thabiti na wepesi wa kupiga mipira mguuni kwake.
Bayern wanaongoza kundi E wakiwa wameshinda michezo yote mitatu wakifuatiwa na Benfica ambao wamewazidi Barcelona alama moja pekee.
Mchezo wa Big Bad Wolf ni moja ya michezo pendwa katika kasino zetu za meridianbet. Ukiachana na tabasamu utakalolipata wakati wa kucheza pia unajiwekea nafasi ya kuwa mshindi wa mkwanja mrefu unaotoka kila baada ya mzunguko kukamilika.


