Borussia Dortimund imeona hakuna uhitaji wa kufanya usajili kwaajili ya kupata mbadala wa Erling Haaland ambaye amekuwa na kiwango bora kabisa tangu atue klabuni hapo.
Mshambuliaji huyo wa kimataifa kutoka Norway amekuwa wa moto tangu atue ligi ya Bundesliga mwezi Januari, amendelea kufurahia maisha akiwa Dortimund kama alivyokuwa Salzburg ikiwa tayari amefunga goli 16 katika michezo 18 hapo BVB.
Paco Alcacer ataachana na Dortimund atarudi tena kunako ligi ya LaLiga kujiunga Villarreal baada dirisha la usajili kufunguliwa.
“Hatujafunga magoli machache msimu huu,” Zorc aliiambia Kicker na vijana hao wa Favre wamefunga magoli 84 katika mechi 34 na wamemaliza msimu wa 2019-20 wa Bundesliga wakiwa nyuma kwa tofauti ya alama 13 nyuma ya wababe wa Bundesliga Bayern Munich.
Zorc anahisi safu ya ushambuliaji ya Favre ambayo inawachezaji machachari kama Jadon Sancho, Thorgan Hazard na kinda Giovanni Reyna ambayo imecheza katika kiwango kizuri kwa msimu wa 2019-20 inajitosheleza haina haja ya kuongeza mchezaji mwingine wa aina hiyo.
Haaland ameripotiwa kuongeza kifungu kwenye mkataba wake wa €75m na kusisitiza hatoondoka BVB ingawa timu za ulaya zimekuwa zikimtolea macho na mchezaji mwenzake Sancho amekuwa akionekana kutaka kuondoka klabuni hapo.
Winga huyo wa England amekuwa akihusishwa na kurudi katika ligi ya Premier League na Manchester United wameripotiwa kuvutiwa na mchezaji huyo.
Dortimund tayari wamejihakikishia huduma ya Thomas Meunier na kinda wa Uingereza Jude Bellingham.
Kwa sababu ya thamani ya pesa yako, kwa kila muamala unaofanya wa kuweka pesa kwenye akaunti yako ya Meridianbet unapata 5% bonasi.
Magdalena
Kama wachezaji waliopo wanatosheleza timu hakuna aja ya Dortmund kusajili tena
Furahav
Haaland ni mchezaji mwenye uwezo mkubwa sana.
Ester jackson
Asante kwa habari hizi za kujitosheleza
Flomena
Winga huyo wa England amekuwa akihusishwa na kurudi katika ligi ya Premier League na Manchester United wameripotiwa kuvutiwa na mchezaji huyo.
Saupha mohamed
Bora wasajili waongeze nguvu
Dorophina
Ni sawa km kikosi kina mtu wa kukava nafasi ya jamaa haina shida
lombo
si lazima kusajir ikiwa kama wanaona wako vzr
Jane Michael
Bora wasajili tu
Ernest
Kweli maana itakuwa matumizi mabaya ya Pesa
christopher
dortmund hawawezag kabisa kukaa na wachezaji wazuri, ataishia bayern hyo siku si nying
Sadick
Kila nikisikia mchezaji Haaland namukumbuka wakala wake mwenye uchu wa fedha Mino Raiola ambaye wakati fulani Alex Ferguson aliwahi kumwelezea kama wakala hatari zaidi barani Ulaya. Mara nyingi Dortmund imekuwa ikipoteza wachezaji wake wazuri kuchukuliwa na Klabu kubwa zaidi#meridianbettz
Zuhura omary kindamba
Watafanya vizuri wakisajili ili timu iwe nzuri
Povel
Halaand yupo kwny msimu Bora Sana hv now
Amiri Kayera
Halland atafany makubw zaid
Johnmary joel
Sioni kama kuna ulazima wa kusajili tena#meridianbett
Theonestina
Halland Yuko vizur.Anawatosha.
Janeflora malisa
Ni vzr maan wanatumia bajet
Gabriel
Kiukwel watakuwa wamefanya maamuz mazur maana ukiangalia bado wako vzur sana kwani Borussia Dortmund, au BVB, ni klabu ya kandada ya Ujerumani. Katika miaka ya karibuni, klabu hii imekuwa ni mpinzani mkubwa wa klabu ya Bayern Munich katika kinyanganyiro cha taji la Bundesliga.
Borussia Dortmund wameshawahi kushinda Kombe la Shirikisho la Ulaya mwaka 1997 ambalo sasa linajulikana kama Champion’s Laeague pamoja na Kombe la washindi wa Ligi za Ulaya mwaka 1966 ambalo sasa linajulikana kama Europa League. Kiwanja chao cha mpira cha Westfahlenstadion ndio kikubwa zaidi katika ligi ya Bundesliga
devotha
Dortmund wanawachezaji wazuri hakuna haja ya kuongeza wengine
Samiah
Wanawachezaji wazuri Dortimund
Genia Sikaluzwe
Dortimundi anawechezaji wazuri na wanajitosheleza
neema hassan
Maamuzi sahihi
Omary lukumbi
Erling halland ni mchezaj chipukiz hatar sana
tumaini
Maoni:wako sahihi kabisa
Neema juma
Sijaona km wameongopa kwa hapo
Njiku
Hii ipo poa sana
Leonard
Wana majembe yakutosha
Fatuma kasomo
Wasajili tu
Zeiyana
Ni wakati mgumu sana wanao Dortmund kocha kama kocha hawezi kuonyesha mazaifu yake mbele ya wachezaji kuondoka kwa haaland hameacha pengo kubwa Dortmund
Angelina
Haaland yuko vizuri itakuwa vizuri kama watapata sain yake
Adelta
Dortmund anawachezaji wazuri
Naona Haina haja ya kuongeza
mwajumah
Wanawachezaji wazuri sana Dortmund#Meridianbettz
Mwanahamisi
Bora wasajili waongeze nguvu
Fatina mfingi
Ni vizur pia
Khadija
Dortimund wana wachezaji wazuri mno#meridianbettz
Tatu
Kama wasipo sajiri mwingine kiwango si kitashuka
Theckla
Yuko sahihi
felister
Kama timu imejitosheleza usajili hauna haja
[email protected]
Bora wasajiri tu
Amani
Kama anawachezaji wakutosha aina haja ya kusajili# meridianbettz
Rehema
Yuko sahihi
Rose kapinga
Wanajiweza Haina sababu ya kusajili tena
farida ahmadi
Bora wasajili wachezaji wengine
Issa
Inabid watafute mbadala endapo akaumia
Itakua shida pia kwa timu
Hope mwaikuka
Fresh tu
David Pere
Halaand bado hazivutii timu nyingi Sana Ndio maana hawapo tayari kutafuta mbadala wake
warda
Kweli Haaland Anajua sana#Meridianbettz