Rais wa Barcelona Joan Laporta amesema kwamba alikuwa na natumaini la kwamba Lionel Messi ngesalia katika klabu ya Barcelona na kuichezea klabu hiyo bure kabla ya kutua Paris Saint-Germain.
Mkataba wa Lionel Messi huko Camp Nou uliacha kufanya kazi mwezi Juni ingawa mazungumzo yalikuwa yakiendelea na ilikuwa ikionekana nahodha huyo wa zamani wa Barcelona angesalia kitu ambacho hakikuwezekana na kuona Muargentina huyo akiondoka kwa uhamisho wa bure.
“Nampenda sana na nina hasira,” Laporta alikuwa kiongea kuhusu Messi katika mahojiano na RAC1. Lakini ikafika kipindi vitu havikuweza kutokea na ilikuwa hali ambayo haikutarajiwa na pande zote.
“Alikuwa na hamu ya kuendelea kuwa na Barcelona mimi na yeye tuna mahusiano yenye nguvu na nilikuwa nikijua kwamba kama tukiwa vyema kiuchumi tungeweza kumfidia lakini haikuwezekana sababu alikuwa na ofa nzuri.
SPACE SPIN NA MERIDIANBET.
Ni Mabingwa pekee Meridianbet wanakupa nafasi ya kushinda zaidi na mchezo wa Space Spin katika kasino bomba za meridianbet. Ni wakati wa kufurahia na kutengeza mkwanja bila kuwaza.


