Maisha ya mchezaji Luke de Jong huko Barcelona yanaonekana kufika mwisho na anajipanga kujiunga na klabu ya Cadiz ya LaLiga.
Mshambuliaji huyo wa kati wa Uholanzi amebaki yeye tu kufanya maamuzi ili dili iweze kukamilika.
Mundo Deportivo wameripoti kwamba bosi wa Cadiz Alvaro Cervera hatimaye anaweza kuipata saini ya De Jong kwani alikuwa akihitaji huduma ya mchezaji huyo kwa muda mrefu.
Tetesi za hivi majuzi zilidai kuwa Diego Costa atakuwa njiani kuelekea klabuni hapo, lakini inaonekana wamepata mtu wao.
De Jong alitua Barcelona kama mchezaji muda anayeweza kuwasaidia mwishoni mwa dirisha la usajili la majira ya kiangazi, lakini kutokana na ujio wa Xavi Hernandez inaonekana wazi kuwa hayupo kwenye mipango ya kocha huyo mpya, akiwa amecheza dakika nane pekee tangu Xavi achukue nafasi hiyo.
Nani hapendi kuwa bingwa na kujishindia mkwanja wa kusahato kuelekea katika sikukuu wiki hii. Mchezo wa Ocean Call kutoka kasino maridhawa za meridianbettz unakupa kila sababu ya kuifanya siku kuu yako kuwa ya kuvutia zaidi.


