Licha ya kukerwa na jinsi msimu wa 2021 wa Formula 1 ulivyomalizika, Lewis Hamilton anatarajiwa kurejea kuchukua kiti chake cha Mercedes kwa kampeni ya 2022.
Muingereza huyo ana kandarasi ya 2022 na 2023, lakini kulikuwa na hofu kwamba anaweza kuachana na mchezo huo baada ya jinsi mizunguko ya mwisho ya Abu Dhabi Grand Prix ilivyoshughulikiwa na mkurugenzi wa mbio Michael Masi. Pia ilikuwa imedaiwa kwamba angeweza kustaafu kama angeshinda michuano ambayo ingekuwa rekodi ya nane ya ubingwa wa dunia.
Hata hivyo, wadadisi wa mambo ya Mercedes wamesisitiza kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 37 hakuwahi kupanga kustaafu endapo atashinda taji hilo na kwamba anaweza kurejea licha ya fainali ya kuhuzunisha aliyopoteza.
Kulingana na The Times, Mercedes wanazidi kujiamini kuwa dereva huyo nyota atarejea. Hivi sasa, yupo katika hali nzuri huko Colorado.
Ni muda wako kujiachia na mchezo maridhawa wa Almighty Aztec katika kasino bomba za meridianbettz. Nafasi ya kutengeneza mkwanja iko mikononi mwako kazi ni kwako.
CHEZA HAPA