Marcus Rashford ameonesha sapoti yake kwa Chris Smalling baada ya mchezaji huyo wa zamani wa Manchester United kuripotiwa kuwa muhanga wa uvamizi wa silaha.

Smallimg na familia yake walisema walikuwa nyumbani huko Appia Anticia katika wilaya ya Roma pale wanaume watatu wakiwa na silaha walipo vunja mala na kutaka wafungue kwa usalama.
Wezi hao waliripotiwa kuchukua saa aina ya Rolex na vito vya thamani na kiasi fulani cha pesa za Smalling.
La Gazzetta dello Sport lilisema mke wa Smalling ndiye aliyepiga simu polisi mida ya 5:00 saa za huko siku ya Ijumaa na uchunguzi umeanzakufanyiwa kazi.
Starika wa Man United Rashford alimtumia mchezaji mwenzake wa zamani ujumbe wa pole kupitia akaunti yake ya Twitter: “Nafikiria kuhusu wewe @chrisSmalling na familia yako pendwa, pole sana kwa tatizo lililokupata, sipati picha unajisikiaje lakini nimatumaini yangu upo sawa.
Smalling aliumizwa hivi karibuni na hakucheza siku ya Alhamisi Roma ilipocheza dhidi ya Ajax katika michuano ya Europa League hatua ya robo fainali mchezo wa marudiano.
Kila mtu ana namba zake za bahati, Meridianbet tunatambua namba zinaweza kukufanya milionea leo. Jilipe kwa namba zako za bahati kila baada ya dakika tano.



Adelta
Smallimg pole Sana
Sarah
Pole yake
dorophina
Rashford amefanya jambo la kiuungwana kabisa
warda
Pole yake wezi sio watu wazuri