Ronaldo Kuwakosa Liverpool Sababu ya Kufiwa na Kichanga

Christiano Ronaldo ataukosa mchezo EPL wa Manchester United dhidi ya Liverpool siku ya Jumanne baada ya kufariki kwa mtoto wake wa kiume baada ya kuzaliwa klabu yathibitisha.

Siku ya Jumatatu nyota huyo wa Ureno alitangaza taarifa za kufiwa kupitia akaunti yake ya Instagram lakini pia alibainisha kwamba mtoto wa kike amezaliwa salama na anaendelea vyema.

Ronaldo na mchumba wake Georgina Rodriguez walikuwa wakitarajia kupata mapacha, lakini waliomba faragha baada ya kupoteza na United sasa wamethibitisha kuwa Ronaldo atachukua muda wa likizo ya huruma.

Taarifa kwenye tovuti yao ilithibitisha habari hiyo, inayosema: “Familia ni muhimu zaidi kuliko kila kitu na Ronaldo anawaunga mkono wapendwa wake katika wakati huu mgumu sana.

“Kwa hivyo, tunaweza kuthibitisha kwamba hatashiriki katika mechi dhidi ya Liverpool kwenye uwanja wa Anfield Jumanne jioni na tunasisitiza ombi la familia la faragha.

“Cristiano, sote tunakufikiria na kuwapa nguvu kwa familia.”


VUNA MKWANJA NA AVIATOR

Maana halisi ya ushindi mkubwa unaipata katika kasino ya mtandaoni ya Aviator kutoka meridianbettz. Andaa kapu la ushindi wa mkwanja na beti kibao za BUREEE.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

SOMA ZAIDI

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.