UEFA itatoa tiketi 30,000 kwa mashabiki wa timu zinazoshiriki fainali za Ulaya za msimu huu kama njia ya kuwashukuru kwa msaada wao wakati wa janga la COVID-19. Washindi wa Fainali ya Ligi ya Mabingwa kila mmoja atapata tikiti 5,000 na jumla ya tiketi 8,000 zitatolewa kwa fainali ya Europa League.
Shirikisho la soka barani Ulaya limethibitisha leo kwamba tiketi 30,000 za bure kwa fainali za Ligi ya Mabingwa, Ligi ya Europa, Europa Conference League na Ligi ya Mabingwa ya Wanawake zitatolewa.
Kati ya tiketi hizo, 6,000 zimetengwa kwa kila fainali ya Ligi ya Mabingwa kwa wanawake na Europa Conference League, na 8,000 za Europa League na 10,000 kwa fainali ya Ligi ya Mabingwa.
UEFA wamesisitiza kwamba vilabu lazima vitenge tiketi hizi kwa “Mashabiki wao waaminifu”.
Rais wa UEFA Aleksander Ceferin alisema: “Mashabiki wa mpira wa miguu ndio tegemeo la mchezo na tulidhani itakuwa njia nzuri ya kutambua magumu waliyopitia kwa miaka miwili iliyopita na jinsi walivyoweza kusaidia timu zao na kuishi na mapenzi yao. hata ukiwa mbali na viwanja vya michezo.
Haijawahi kuwa rahisi hivi kwenye safari yako ya kuvuna mkwanja, kasino maridhawa ya meridianbettz inakuletea mchezo wa Emoticoins unaokupa nafasi ya kufanya safari yako kuwa rahisi zaidi. Wakati ni wako nafasi ni yako na Emoticoins.


