Simba Yatoa Kipigo cha Mbwa Koko

Klabu ya Simba inayonolewa na Kocha Mkuu, Sven Vandenbroeck leo Agosti 22, imeibuka na ushindi wa mabao 6-0 mbele ya Vital’O ya Burundi kwenye mchezo wa kimataifa wa kirafiki uliochezwa Uwanja wa Mkapa.

Mchezo wa leo ulikuwa na lengo la kutambulisha wachezaji wapya pamoja na jezi itakayotumika kwa msimu wa 2020/21.

Ushindani ulikuwa mkubwa kipindi cha kwanza ambapo iliwabidi Simba wasubiri mpaka dakika ya 43 kupata bao la kwanza kupitia kwa Bernard Morrison ambaye alimaliza kazi ya pasi ndefu ya Larry Bwalya ambaye naye ni nyota mpya wa Simba.

 

Dakika mbili mbele, Morrison alitengeneza pasi kwa nahodha wa Simba John Bocco ambaye alipachika bao la pili dakika ya 45.

Simba ilikwenda mapumziko ikiwa mbele kwa mabao 2-0 huku Vital’O ikiwa haijaambulia bao ndani ya dakika 45.

Kipindi cha pili, Simba ilifanya mabadiliko kwa wachezaji wake wote ambao walianza kikosi cha kwanza ambao ni Aishi Manula, Shomari Kapombe, Gadiel Michael, Ibrahim Ame, Joash Onyango, Jonas Mkude, Hassan Dilunga, Larry Bwalya, John Bocco, Said Ndemla na Morrison.

Nyota walioingia ilikuwa ni pamoja na Beno Kakolanya ambaye aliumia dakika ya 64 na kumpisha Ally Salim, Mohamed Hussein,Keneddy Juma,Erasto Nyoni,Gerson Fraga,Mzamiru Yassin,Ibrahim Ajibu,Clatous Chama,Cris Mugalu, Charlse Ilanfya na Mirsaj Athuman.

Kikosi cha pili kilipachika mabao manne ambapo bao la tatu lilipachikwa na Chama dakika ya 56 akimalizia pasi ndefu ya Ajibu ambaye alifunga bao la nne dakika ya 75 kwa pasi ya Chama kisha bao la tano likapachikwa na Mugalu dakika ya 77 kwa pasi ya Miraj huku msumari wa mwisho ukipachikwa na Ilanfya kwa pasi ya Mohamed Hussein.

Sven amesema kuwa ulikuwa ni mchezo mgumu na mzuri huku wachezaji wake wakionyesha kile ambacho amewafundisha jambo ambalo linampa picha ya kikosi chake kuanza kufanya vizuri ndani ya ligi na mashindano mengine.


Drops and Wins!

Umeijua hii? Ni promosheni kabambe ya ushindi kwenye Kasino ya mtandaoni ya Meridianbet! Unaweza kushinda hadi Euro 2,000,000 leo.

Soma Zaidi

44 Komentara

    Kile kipigi sio cha kubahatisha aisee

    Jibu

    Simba walijua kumchapa mtu bhana sio kwa bao zile wametufurahisha sana mashabiki wao sasa watani wetu wa jadi wajiandae mwezi wa 9 tutakavyowachakaza #Meridianbettz

    Jibu

    Mmeenda kuleta timu mbovu.ili tuwaone vidume.tumewashtukiaaaa.timu uko kwao imeshuka daraja

    Jibu

    Jana walijua kubahatisha..

    Jibu

    kilikua cha kawaida tu

    Jibu

    Simbaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa sitaki kusema mengi wenyewe waneona kuwa sisi ni watu wabaya jamani simbaaaaaaaaaaaa nasikia raha hadi nahisi kulia simbaaaaaaaaaa ni baba lao maana mambo yalianzia kwenye show tulimaliza kila kitu baraka zote zimeachwa n mondiiiiii

    Jibu

    Simba Jana wametufoke si kwa mabao yale

    Jibu

    Simba sio ya mchezo mchezo Yani tulijua tyu yang mtaongea Ila nn subir muone tumeleta Tim mbov au nn!!

    Jibu

    Kikubwa. Duwa tunataka wakutane na wajadi wao tuone mambo yakoje kutokana na usajili wao

    Jibu

    Simba baba lao ni nouma Sana hakuna kama Simba

    Jibu

    Maoni:simba wana kikosi kizuri sana msimu huuu atari

    Jibu

    Nadhani ilitakiwa wafunge mengi zaidi maana kila kipindi walicheza wachezaji tofauti hivy walikuwa na ari mpya na nguvu mpya#meridianbettz

    Jibu

    Simba jana imenifurahisha sana mashabiki wa simba oyeeee#meridianbettz

    Jibu

    Me sioni haja ya leo simba kushangilia ushindi ambao timu umeichagua wenyew kucheza nayo na mmeilipa mwenyew ni sawa mwanamke hanunue mwanaume alafu Nazi hafanye mwenyew na ukiangalia timu yenyew uko kwao imeshuka daraja..!yani mashabiki wote wa simba jana walikua hawana hata haja ya kushingilia yani kama wamepasha misuli tu wanaomba dua hiyo siku wakikutana na wanaume ila mashabiki viele ele ndio wanao piga kelele

    Jibu

    Mashabiki wa simba Jana tulifurahi sanaaaaaaaaaaa@meridianbettz

    Jibu

    Wamebahatisha amna lolote wamewaachia tu kwasababu mechi ilikuwa ya kirafiki

    Jibu

    THIS IS SIMBA

    Jibu

    Simba haina mpinzani.

    Jibu

    Simba sijaona ajabu kumfunga vital’o

    Jibu

    Simba walitisha Jana hu moto waendelee nao msimu ujao

    Jibu

    Kabisa kile kibigo kilikuwa si chakitoto kilikuwa chambwa mwitu kwakweli Mambo yalikuwa moto huwanja wamkapa akuna Kama zimba mashabiki fulu kufurahi yani

    Jibu

    Kama namuona vile Baraka Mpenja akitangaza mauaji haya ya kikatili kutoka kwa Simba

    Jibu

    Simba aina mpinzani

    Jibu

    Simba haina mpnzani

    Jibu

    Naipenda cmba mpo vizuri

    Jibu

    Simba imepata mchekea tu jana

    Jibu

    Simbaaaaaaa wamejipanga

    Jibu

    Mmmh Simba wamekutana na vilaza tuu

    Jibu

    Simba wako vzur

    Jibu

    Simbaaaa juuuu

    Jibu

    This is SIMBA next LEVEL

    Jibu

    Simba ni next level…jana walijua kutapa raha mashabiki zao

    Jibu

    Simba babalaooo

    Jibu

    Haya bhana wanasimbaa tuwape hongera zenu khaa.mmetisha

    Jibu

    Hongera yao.

    Jibu

    jambo ambalo linaleta picha ya kikosi kuanza kufanya vizuri ndani ya ligi na mashindano mengine, hongereni wanasimba.

    Jibu

    Goli kama hizi anahitajika kufugwa Yanga#Meridianbettz

    Jibu

    simba wana kikosi kizuri sana na wanajituma sana na kinajituma sana tena sana sisi wanakamati tunaelewa

    Jibu

    Hongera yao

    Jibu

    Simba hapo ni Kama wamejitekenya wenyewe na kuanza kucheka wenyewe hauwezi kumkarbisha mgen then umpatie kila kitu had hela alafu umwambie akupige

    Jibu

    timu makini na watu makini big up

    Jibu

    Simba kama simba wababe!!!

    Jibu

    Kama namuona vile Baraka Mpenja akitangaza mauaji haya ya kikatili kutoka kwa Simba

    Jibu

    Simba baba laooo

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.