Romelu Lukaku amemuagiza mwanasheria kuangalia hali ya hewa juu ya uwezekano wa kurejea katika klabu yake ya zamani ya Inter baada ya kuwa na msimu mgumu na Chelsea.

Mazungumzo ya leo yanahusu kupanga mpango wa mkopo ambapo Lukaku anakubali kupunguza mshahara wake kwa karibu asilimia 40 ili kuwezesha kurejea San Siro.
Hata hivyo, inaaminika kuwa The Blues huenda wakataka ada kubwa ya mkopo kati ya €12m na €24m ambayo inaweza kuonekana kuwa shida nchini Italia.
Chaguo la kumnunua linaweza kujumuishwa au muundo unaoruhusu malipo yote kwa misimu kadhaa.
Chelsea bado hawajatoa orodha kuhusu wachezaji wanaoondoka ambao watachagiza mipango ya uhamisho ya Chelsea majira ya kiangazi lakini sasa wanatarajiwa kukamilisha wiki hii.
SHINDA Samsung A32 ukiwa na mchezo wa Aviator kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet! Kwea pipa ukusanye zawadi zako pamoja na ushindi mnono wa mkwanja!


