Atletico Madrid wameikataa ofa yenye thamani ya paundi milioni 78 (€85m) kutoka klabu ya Manchester City kwaajili ya kumsajili Jose Gimenez rais wa klabu hiyo ya LaLiga Enrique Cerezo amethibitisha.
Gimenez mwenye umri wa miaka 25 amekuwa akihusishwa kujiunga na City na AS iliripotiwa mapema mwezi huu kwamba Atletico Madrid wameamua kuipiga chini ofa ya pesa ndefu kutoka katika klabu hiyo ya Premier League.
Cerezo alithibitisha kwamba miamba hiyo ya LaLiga ilipokea ofa kutoka kwa Manchester City , lakini wameamua kumbakisha mlinzi huyo, ambaye siku kadhaa zilizopita aliripotiwa kuwa na maambukizi ya virusi vya Corona.

‘Tulipokea ofa,” aliiambia El Transitor.
“Lakini Gimenez mchezaji mzuri na tunavutiwa kuwa na wachezaji wazuri katika timu yetu.”
Baada ya kumaliza katika nafasi ya tatu kwenye LaLiga msimu uliyopita, Atletico ambao wamekubali kusaini dili na nyota kutoka Barcelona, Luis Suarez- wataanza mbio za kuwania ubingwa wa LaLiga wataikaribisha Granada katika dimba la Wanda Metropolitano.
Wakati msimu mpya wa LaLiga unatarajia kuanza bila mashabiki halli yakuwa kuna janga la COVID-19, Cerezo anatumaini mashabikiwataanza kuruhusiwa hivi karibuni.
“Tuna tumaini kwamba uma utaanza kuruhusiwa kuingia viwanjani kabla msimu haujaisha,”alisema Cerezo.
FURAHIA KASINO YA MTANDAONI
Tembelea ardhi ya maajabu ushangazwe na mengi ikiwa ni pamoja na urahisi wa kujipatia utajiri kupitia Kasino ya Meridianbet.


magdalena
atletico iyo ofa msiikubali maana uyo mtu ana mchango mkubwa na timu wakimchukua watakuwa wamewapa pengo kubwa sana
Mwajumah
Atletico msimtoe uyo kijana maana mtakua na pengo kubwa sana kwenye timu bola abaki tu apoapo
Elika
Asitoke hapo mbona anamchango mkubwa sana
Fatina mfingi
Mbona mchago wake Ni mkubwa wamuache bhan na wasikubali hiyo ofa ya man city
Dorophina
Gimenez awezi kwenda man city
Sauda
Mikwara tu, hawezi kuondoka..
Adelta
Msikubali hiyo ofa kwa yeye anamchango mkubwa kuliko hiyo ofa yao
Ernest
Mancity wanapata vikwazo vingi sana kwenye usajili mwaka huu
Caroline
Mancity kazi wanayo mwaka huu
Angelina
Gimemezi yuko vuzuri wasimtoe
Lydia Emmanuel Magoti
Maneno tuu hayo
Nasra
Kazi ipo kwa man city
Rehema
Asante kwa taarifa
Sadick
Man City inahitaji sana beki ingawa mfumo wa Guardiola wa pass nyingi kuanzia langoni na kumiliki mpira muda mwingi pengo la mlinzi halionekani sana#meridianbettz
aisha
Duuh man city sijui wanafeli wapi kwenye usajili
Janeflora malisa
Asnt Kwa taarif
Venerose
Safi
Tatu
Man city wanazingua
Khadija
Hawezi kuondoka kwenda man city
Rehema Dickson
Asitoke hapo mbona anamchango mkubwa sana
Saupha mohamed
Abaki mchango wake mkubwa
Neema
Kwaninii sasa aondoke. Kutakuwa na pengo kubwa
Fatuma kasomo
Aendele anapotaka
Johnmary joel
Kwakweli wanachangamoto kubwa man#meridianbett
Amiri Kayera
Wamemzuia ili kuwasaidia
Sabrina
Gimenez aendelee kikipiga hapo hapo Atletico
Gabriel
Gimemezi Wamemzuia ili kuwasaidia
Samiah
Safi
Zeiyana
Atletico haiwezi kumuuza gimenez amekua na masaada mkubwa sana pale clabuni
Rose kapinga
Hatarii sana
Hopemwaikuka
Msikubal kabsa jembe hilo
Issa
City waongez dau simeon huwa ana kawaida ya kumnga’ngania mchezaji
David Pere
Atletico iyo ofa msiikubali maana uyo mtu ana mchango mkubwa na timu wakimchukua watakuwa wamewapa pengo kubwa sana