Chozi la Suarez kwa Barcelona

MAMA mzazi wa Luis Suarez aitwaye Sandra alikuwa ni mfagizi katika moja ya kituo cha mabasi katika kitongoji cha Tres Cruzes Jiji la Montevideo nchini Uruguay na hakuwahi kukata tamaa kuhusiana na mwanaye kwamba atakuja kuwa mtu mkubwa na maarufu siku moja duniani.
Katika kitabu chake cha Luis Suarez, Crossing The Line, Suarez ameelezea namna Sandra alivyokuwa akihangaika na watoto wengi aliokuwa akiishi nao licha ya umasikini wake na kufanya asiwe na muda wa kumuuliza kuhusiana na shule hasa maendeleo yake.
Pamoja na hivyo, ameeleza namna mama yake alivyoendelea kumpa moyo na kumuasa kuendelea kupambana kwa kile anachokiamini kwa kuwa hakupenda kumpangia. Baba yake mzazi, Rodolfo Suarez alikuwa ni mwanajeshi, baadaye akaamua kuondoka jeshini na maisha yakawa magumu zaidi hadi kufikia kuanza kujitafutia riziki kwa kufanya kazi katika kiwanda cha biskuti na baadaye kuamua kujihusisha na ujenzi. Kuna wakati Rodolfo hakuwa hata na fedha ya kujilipia kodi ya pango tu na kulazimika kulala katika eneo walilokuwa wakifanya ujenzi ili kujisitiri.
Suarez anazungumzia namna umasikini ulivyowafanya wazazi wake washindwe kwenda kumuunga mkono wakati akienda mazoezini katika klabu ya watoto ya Nacional, moja ya klabu maarufu nchini Uruguay. Pamoja na hivyo, Suarez ameeleza anavyoendelea kuwashukuru wazazi wake kwani licha ya kutomuunga mkono kwa vitendo walikuwa wakimpa maneno ambayo yalimfanya aendelee kupambana bila ya kuchoka na mwisho anamtaja mkewe Sofi Balbi kuwa ndiye shujaa wake.
Suarez na Sofi sasa wana watoto watatu, binti Delfina (alizaliwa 2010) na wavulana wawili, Benjamin (alizaliwa 2013) na Lauti, aliyezaliwa 2018. Walianza kuwa wapenzi Suarez akiwa na umri wa miaka 15 na Sofi akiwa na 13.
Mshambuliaji huyo mtukutu sasa ana umri wa miaka 13 na chanzo cha mafanikio yake ya mpira ni Sofi na ndiyo maana anamuona ni shujaa wake lakini mji ulio katika historia ya maisha yake ni Barcelona.
Huenda hapa inakuwa ni nafasi nzuri ya kujua kisa cha yeye kufikia kumwaga chozi wakati anaondoka katika klabu hiyo na kwenda kujiunga na Atletico Madrid ambao ni moja ya wapinzani wakubwa wa Barcelona kutoka katika Jiji la Madrid. Baada ya kocha mpya wa Barcelona, Ronald Koeman kuonekana hana mpango wa kumtumia au hana mpango naye, ikaelezwa atajiunga na Juventus ya Italia na kuungana na Cristiano Ronaldo.
Akiwa katika hatua za mwisho, ikabainika kuwa alifanya udanganyifu wakati akitafuta uraia wa Italia ambao anao. Hivyo ikawa ni kesi ambayo mwisho ilionekana anastahili kubaki nao lakini kukawa na ugumu tena kujiunga na Juve. Ofa ya Atletico, mwisho imefanikiwa kama mchezaji huru lakini mwisho aliangua kilio kama mtoto akijua anaondoka Barcelona.
Wengi wanaweza kudhani ni mapenzi pekee na klabu hiyo ambayo wana kauli mbiu yao “Zaidi ya Klabu”. Suarez lazima atakuwa anakumbuka maisha ya Barcelona ambayo alijiunga nao mwaka 2014 akitokea Liverpool na kufanikiwa kuichezea mechi 191 na kufunga mabao 147, hivyo kuandika rekodi ya kuwa mmoja wa washambulizi hatari zaidi waliowahi kuichezea Barcelona.

Itaendelea..


Beti kwa Kitochi Kushinda 300,000,000!

Unajua kuwa unaweza kushinda milioni mia tatu kwa buku tu? Ndiyo! Unaweza kushinda kwa kupiga *149*10# na kubashiri. Ingia mchezoni!

Soma Zaidi

32 Komentara

    🔥

    Jibu

    Uenda suarez ndoto zake zilikuwa ni kutumikia barca adi atakapostaafu soka

    Jibu

    suarez alikuwa anataka kuitumikia barca kama messi lakini ndoto zake zinaonekana hazikutimia

    Jibu

    Aki yake Suarez kutoa chozi alikuwa anataka kuitumikia Barcelona mwanzo mwisho kwaio kila chenye mwanzo kina mwisho

    Jibu

    Suarez ana mapenz na Clab yake ndiyo maana alikuwa hataki kuhamia popote.

    Jibu

    Ni historia ya kusikitisha sana na yenye mafunzo kwa wote ni kutokata tamaa ya maisha yako.

    Jibu

    Alikuwa mzalendo na clab yake

    Jibu

    Dahh Asante kwa taarifa

    Jibu

    Inaonekana wamemkatisha Suarez ndoto yake ya kutaka kuitumikia Barca mpaka mwisho wa maisha yake

    Jibu

    Suarez alikuw na wakat mzur Barcelona na kombineshen yake na mess ilikua mahir kwenye ufungaji

    Jibu

    Usijal hata huko utakua poa tu

    Jibu

    Suarez ameshindwa kutimiza ndoto yake

    Jibu

    Gud news

    Jibu

    Hayo ndio maisha ya mpira Suarez kila kitu kinaenda na wakati hata sehemu huliyopo ni sahii pia hinaweza ukafanya mkubwa kushindwa hata ya pale na ndio hinavyo kua kila kiongozi anapoingia kwenye madaraka yake lazima hapange yake ili kujenga kitu kiwe kwenye ubora hanao taka yeye yote kwa yote nia yake kukijenga kikosi kiwe kwenye ubora

    Jibu

    Gud news

    Jibu

    suarez ndoto zake zilikuwa ni kutumikia barca

    Jibu

    Barcelona wamekatisha malengo ya suarez

    Jibu

    Km mchezaj maisha popot tegemea

    Jibu

    Amefanya makubwa barca na kombineshen yake na mess ilifanya atupie
    Magoli sana

    Jibu

    duh hatar

    Jibu

    Sio kila ndoto zinatimia hata kama alikua na mpango wa kumalizia mpira barca anatakiwa kuangalia alipo sasa asitazame alipotoka

    Jibu

    kiukweli Barcelona wamemkatili Suarez

    Jibu

    Mashabiki tunashukuru kwa makala nzuri

    Jibu

    Suarez anaipenda club yake

    Jibu

    Suarez ameshindwa kutimiza ndoto yake

    Jibu

    Gud news

    Jibu

    Moyo wa Suarez bado uko barca

    Jibu

    Good

    Jibu

    Aaw 😥

    Jibu

    Historia yake inatia motivation

    Jibu

    Suarez alikuw na wakat mzur Barcelona na kombineshen yake na mess ilikua mahir kwenye ufungaji

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.