Lille na Gourvennec Waridhiana Kukatisha Mkataba

Klabu ya Lille imefikia maridhiano ya pande zote ya kukatisha kandarasi na aliyekuwa kocha wa klabu hiyo Jocelyn Gourvennec klabu ilithibitisha siku ya Alhamisi.

Lille na Gourvennec Waridhiana Kukatisha Mkataba
Jocelyn Gourvennec

Gourvennec alichukua mikoba ya kuinoa klabu hiyo ya Ligue 1 baada ya kuondoka kwa kocha aliyewapa taji la Ligue 1 Christophe Galtier ambaye alijiunga na Nice pia.

Lille wamefikia uamuzi huo kufuatia muenendo mbaya wa timu kwa kumaliza nafasi ya 10 wakiwa wamekusanya alama 55 msimu wa 2021-22.

Klabu ya Lille ilimtakia kila la kheri Gourvennec kwa taarifa iliyoandikwa “Tunamshukuru Jocelyn Gourvennec kwa ushirikiano wake, kujitolea kwake na taaluma yake kwa msimu wa 2021-22 akiwa amefanikiwa kutwa taji la French Super Cup”.

Lille na Gourvennec Waridhiana Kukatisha Mkataba

LOSC wamefikia uamuzi huo baada ya kocha huyo kushindwa kuendeleza kile walichokipata msimuwa 2020-21, wakitolewa katika raundi ya 16 na Chelsea katika michuiano ya Ligi ya Mabingwa.

Taarifa za awali zinadai kwamba kocha wa zamani wa Shaktar Donetsk na Roma Paulo Fonseca ndiye anye pi8giwa upatu wa kurithi mikoba ya Gourvennec.


ALIYA’S WISHES

Bila shaka unatamani ushindi mkubwa, vipi kuhusu kujaribu Sloti hii ya Aliya’s Wishes? jaribu ushinde sasa.Kasino ya Mtandaoni

CHEZA SASA

Acha ujumbe