Roberto Mancini ameelezea masikitiko yake kwa kumuuona Mario Balotelli muonendo wake kutoka kuwa kijana wa dhahabu hadi kuwa mchezaji wa thamani ya chini.
Bosi wa timu ya Italia Mancini alimpa nafasi Baloteli katika ligi ya Serie A kipindi anainoa Inter kwa wakati huo Baloteli alikuwa na umri wa miaka 17 mwezi Disemba, 2007 na mchezo wake wa kwanza kwa Azzurri ulikuwa kabla hajafikisha miaka 20.
Baloteli alimfuata Mancini katika ligi ya Premia wakati Machini alipokabidhiwa mikoba ya kunoa timu ya Manchester City, sehemu ambayo Balotelli aliweza kuonesha kipaji chake lakini alikuwa akikabiliwa na mambo mbalimbali ya nje ya uwanja.
Baada ya kuvichezea vilabu mbalimbali kama vile Inter Milan, Liverpool,Nice, Marseille na Brescia sasa amekuwa bila timu akiwa na umri wa miaka 30.
Akiongeakatika hafla ya moja ya michezo siku ya Alhamisi, Mancini aliongea juu ya Balotelli: “Nasikitika sana kumuona katika hali hii, akiwa na umri wa miaka 30 ilitakiwa awepo katika nafasi nzuri ya ukubwa katika soka na ilipaswa atumike katika timu ya taifa.
“Nampenda natumaini atapata jambo zuri .”
Kwa mapenzi aliyonayo Mancini kwa Balotelli alimuita katika kikosi cha timu ya taifa mara baada ya Mancini kukabidhiwa Azzurri mwaka 2018 baada ya kutoitwa katika timu hiyo miaka mingi lakini mshambuliaji huyo hakuweza kuilinda nafasi hiyo.
Balotelli alikuwa akihusishwa na vilabu mabimbali baada ya kuondoka Brescia msimu uliyopita na ilisemekana mapema mwezi Oktoba angejiunga na timu mpya “ndani ya wiki chache”.
Tunazungumzia mkwanja wa Tshs.160,000,000! Kupitia Kasino ya Mtandaonii ya Meridianbet unaweza kuwa milionea wakati wowote.



Carolyn
Balotel ujeuri ulizidi ndo maana akashuka kiwango
Sauda
Baloteli akiongeza juhudi ataimarisha kiwango chake.
Mwajumah
Baloteli ni mchezaji mzuri sana ila anakitabia Cha ujeuri jeuri akibadilika atakua mchezaji bora sana
Mwanahamisi
Balotel awe mpole asionyeshe makucha yake ktk uchezaji
Fatina mfingi
Balotel kiwango chake kimeshuka san kwa ss!! Inabid abadilike
Tatu
Nyota ya balotel imepotea awiki kama zamani
Dorophina
Baloteli kwa Sasa kiwango chake kimeshuka sana
Lydia Emmanuel Magoti
Yupo sahii Mancini anacho kizungu mza kwa Balotelli
Angelina
Balotel jeuri sana abadilike
Adelta
Balotel awe na subra Mambo yatakaa sawa tu
Khadija
Asante kwa taarifa
Ester jackson
Balotel mbabe sana huyo ndio mana kiwango chake hakiwezi kukua kwa urahisi kutokana na tabia yake hata kama anacheza vizuri
aisha
Balotel ili kiwango chake kirudi kama zamani anatakiwa kuwa na nidhamu ya hali ya juu
Sabrina
Baloteli hana jipya kipaji kimefujika
Elika
Barotel ndo bas tena kashapotea
Ernest
Nidhamu imempoteza mapema Balotelli kwenye Ramani ya Soka, Wachezaji wachanga wanakitu cha kujifunza kupitia Balotelli.
warda
Sijui kwa nini Balotelli huwa Hakui
zeiyana
barotel kama hangekua kwenye gemu karne hii ya sasa hangekua mabali sana bado historia yake haiwezi kufutika kwenye ulimwengu wa soka na bado pia mri wake hunaruusa nafasi yake bado haijapata mbadala wake
Amani Maeda
Balotelli anasumbuliwa na dharau na kutojali yeye ni nani katika kazi yake ndo maana anatangatanga sasa.
Hopemwaikuka
Sifa zilimponza
Issa
Baloteli amekua mchezaji asie na bahati sana
Povel
Nidhamu ndo inapoteza soka la mario balotelli mapema
Saupha mohamed
Baloteli amepootea saiv
Fatuma kasomo
Gud news