Okrah: Nataka Kufunga Sana Msimu Huu

Kiungo wa Simba Augustine Okrah amefunguka kuwa anataka kuwa mfungaji bora wa timu hiyo ili kuwapa furaha mashabiki na kuwa mchezaji wa kutumainiwa.

Okrah amefunguka hayo baada ya kufunga bao lake la kwanza tangu ajiunge na timu hiyo kwenye mchezo wa kirafiki uliochezwa wikiendi iliyoisha dhidi ya Ismailia na kutoka sare ya bao 1-1 na yeye akifunga bao la Simba.

Akizungumzia matarajio yake ndani ya kikosi hicho Okrah ambaye ni raia wa Ghana alisema anafurahi kuona kuwa ameanza vizuri Maisha yake ndani ya timu hiyo na anaamini kuwa anakwenda kufanya vizuri zaidi akiwa na uzi wa klabu hiyo.

“Huu ni mchezo wangu wa kwanza, nadhani natakiwa kuimarika zaidi na kufunga zaidi kwa ajili ya mashabiki zangu wa Simba.

“Nashukuru pia kwa kuanza Maisha yangu vizuri kwenye timu hii na naamini kuna mambo mazuri zaidi na kwenda kuyaona nikiwa na timu hii,” alisema.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.