Kocha wa timu ya taifa ya Hispania, Luis Enrique amekiri kuwa uwezo wa kinda wa klabu ya Barcelona na timu ya taifa ya Hispania, Ansu Fati, wa kucheza mpira, kujiamini, kutengeneza nafasi ni mkubwa sana na usio wa kawaida.
Kinda huyo mwenye umri wa miaka 17 tu anakichezea kikosi cha Hispania kwa mara ya kwanza katika mashindano ya mataifa ya UEFA na ameonesha kiwango kikubwa sana. Fati alifunga goli katika mechi yake ya pili tu na kikosi cha Hispania siku ya Jumapili.
Hispania waliwakabili Ukraine katika mtanange huo na walijipatia goli la kwanza mapema kabisa kutoka kwa Sergio Ramos kwa mkwaju wa penati. Goli la pili la Hispania lilifungwa na Fati dakika ya 32 ya mchezo, hadi dakika 90 zinamalizika, Hispania 4 na Ukraine 0.
Ansu Fati, aliyecheza dakika zote 90 katika mchezo huo, alionwsha kiwango cha kuridhisha na kumfurahisha kocha wake Luis Enrique. Pamoja na kufunga goli lake la kwanza na timu ya taifa ya Hispania, Fati alitengeneza nafasi mbili, kupiga mashuti sita na ‘dribbles’ sita ambazo ni nyingi kuliko mchezaji yeyote aliyecheza mechi hiyo!
Baada ya mchezo huo kumalizika, Enrique hakuwa na maoni mengine kwa Fati zaidi ya kumsifia kwa kiwango chake na kuwa hajaonesha ‘utoto’ kama ilivyotarajiwa kutokana na umri wake mdogo.
“Wakati tunaita kikosi hatukuangalia sana umri wake. Ilikua wazi kuwa, kutokana na umri wake, Fati atacheza vibaya mara nyingine, atafanya makosa ya wazi kabisa. Tuliamini hiyo yote itakua ni sehemu ya kujifunza kwake, lakini alichokuja kukionesha ni tofauti kabisa na matarajio,” Enrique alisema.
“Amecheza kwa kujiamini na utulivu wa hali ya juu. Ninafurahi kumuona mwenye furaha hivi. Natumaini atafanya makubwa zaidi ya haya.” Enrique akiendelea kumwagia sifa Ansu Fati
Hispania watazikabili Ureno na pia Switzerland katika hatua inayofuata ya mashindano hayo.
SHINDA NA MERIDIANBET!
Tengeneza pesa kidijitali kwa kubashiri mbio za farasi hapa Meridianbet! Chagua nani ashinde, unakusanya mkwanja.


Flomena
Baada ya mchezo huo kumalizika, Enrique hakuwa na maoni mengine kwa Fati zaidi ya kumsifia kwa kiwango chake na kuwa hajaonesha ‘utoto’ kama ilivyotarajiwa kutokana na umri wake mdogo.
rama
safi sana kijana mwazo mzuri huo
Zeiyana
Ni kweli hanacho sema enrigue ukiangalia ansu amekua na mabadiliko makubwa sana
Adelta
Enrique Yuko vizuri na anajiamini@meridianbettz
Mwanahamisi
Safi sana
felister
katika mashindano ya mataifa uefa ameonyesha kiwango cha juu sana
Antony Luseno
Kwa mwendo uwo alionao naona ukifika mbali
Ernest
Messi the GOAT alishasema kuwa kijana anafuture kubwa sana huko mbeleni endapo tuu ataongeza juhudi na maarifa.
Shani
Ansu fat ni mchezaji atakaekuwa hodari the msimu miwili
Povel
Kwl Ansu FATi amekwisha iva yupo kwny ubora sana
Sabrina
Ansu Fat ni mchezaji mzuri alafu umri wake unaruhusu.
magdalena
kijana alifanya vizuri sana ila aendelee kuonesha juhudi nyingi zaidi ili aweze kufikia mbali
Elika
Kijana yuko vizuri sana..hongera sanaaa
Furahav
Yuko vizuri.
Lydia Emmanuel Magoti
Kijana yupo vizuri azidi kupambana tuuu atafika panapo stairi
Fatina mfigi
Kijana yupo vizur
aisha
Umefanya vizuri uendelee hivyo hivyo
Tatu
Kijana yupo vizuri sana
Hidaya
Apambane tu atafika anapotaka
Sadick
Anaweza kuwa Messi ajae wa Barcelona. Kuna baadhi ya chipukizi ambao hupata umaarufu mapema hupotea mapema kutokana na kulewa umaarufu#meridianbettz
Khadija
Safi sana kijana#meridianbettz
Mwajumah
Ansu fat ni mchezaji mzuri sana akaze buti azid kukuza kipaji vizuri#Meridianbettz
Hope mwaikuka
ANSI anajua wajibu wake ni nn so namuaminia sana
lombo
asante meridianbet kwa habar moto moto
Shafii
Ansu yuko vizuri sana .
Theckla
Anajua sana
Issa
Ansu kinda ataekuwa poa pale barca
Salma ngende
Yupo vizuri kijana
Amiri Kayera
Ni nyota anaekuja Kwa kasi
Saupha mohamed
Safi sana
Rehema
Yuko vizuri
Gabriel
kikosi hatukuangalia sana umri wake. Ilikua wazi kuwa, kutokana na umri wake, Fati atacheza vibaya mara nyingine, atafanya makosa ya wazi kabisa. Tuliamini hiyo yote itakua ni sehemu ya kujifunza kwake, lakini alichokuja kukionesha ni tofauti kabisa na matarajio,” Enrique alisema.
Janeflora malisa
Yupo vzr
Latifa juma mohamed
Kwa mwendo uwo alionao naona ukifika mbali
Sauda
Vizuri sana kijana
Rose kapinga
Kazi nzuri!!
Nasra
Safi sana
Tumaini kasalile
Yuko pw
Samiah
Yupo sawa
David Pere
Baada ya mchezo huo kumalizika, Enrique hakuwa na maoni mengine kwa Fati zaidi ya kumsifia kwa kiwango chake na kuwa hajaonesha ‘utoto’ kama ilivyotarajiwa kutokana na umri wake mdogo.