Calhanoglu ambaye bado ana mkataba na AC Milan atatimka klabuni hapo wiki ijayo pale tu mkataba wake utakapokamilika. Calhanoglu ametumikia AC Milan kwa miaka minne na alikataa dau la Euro Milioni 4 lililotolewa na timu hiyo.
Hakan Calhanoglu alijiunga na AC Milan akitokea klabu ya Bayer 04 Leverkusen mwaka 2017 na toka hapo amecheza mechi 43 na kutoa pasi za magoli 12 na kufunga tisa katika michuano yote akiwa na AC Milan.
Katika michuano ya Euro 202, Hakan Calhanoglu amecheza mechi tatu tu na kutoa pasi moja tu ya goli. Mchezaji mwenye asili ya ujerumani na Uturuki ameamua kuchezea Uturuki na alikuwa miongoni mwa wachezaji tegemezi kutokana na timu aliyotoka.
Usajili huo wa Inter unaelekea kufanya maboresho eneo la ushambuliaji la Inter Milan kutokana na tetesi mbalimbali zilizo kuhusu wachezaji mbalimbali wa timu hiyo ambao wanaweza kununuliwaa katika majira haya ya joto!