Klabu ya Chelsea imeripotiwa kuomba kikao na wakala wa mchezaji anayekipiga kwenye klabu ya Real Madrid Eder Militao kuhusu uwezekano wa kupata saini yake majira ya kiangazi.
Awali klabu ya Chelsea kwenye majira ya baridi walihusishwa kutaka saini ya mlinzi huyo kutoka klabu ya Real Madrid lakini hakuweza kufanikiwa kupata huduma yake, na wakahamia kwa mlinzi wa klabu ya Sevilla Jules Kounde, nako huko wakatoka patupu.
Chelsea iko mbioni kuwapoteza walinzi wake watatu ambao mikataba yao inaisha majira ya kiangazi, Antonio Rudiger, Cesar Azpilicueta na Andreas Christensen ikiwa klabu ya Chelsea itashindwa kufanya makubaliano nao basi wataondoka bure wote.
Militao hakuwa na kasi nzuri wakati anasajiri na klabu ya Real Madrid kutokea klabu ya FC Porto ya nchini Ureno, lakini kwa sasa ameonesha umuhimu mkubwa na klabu ya Chelsea itabidi itumie nguvu kubwa kuweza kumuondoa Madrid.
Mpaka sasa matajiri wa London “The Blues” bado haijafanikiwa kupata jibu lolote kutoka kwa wakala wa Eder Militao kuhusu kuzungumzia uhamisho huo.
Haijawahi kuwa rahisi hivi kwenye safari yako ya kuvuna mkwanja, kasino maridhawa ya meridianbettz inakuletea mchezo wa Emoticoins unaokupa nafasi ya kufanya safari yako kuwa rahisi zaidi. Wakati ni wako nafasi ni yako na Emoticoins.