Chelsea Wahamia kwa Cesare Casadei

Klabu ya Chelsea bado inaendelea na mazungumzo ya kutaka kumsaini mchezaji kinda wa klabu ya Inter Milan baada ya nazungumzo ya msingi kuhusu uhamisho huo kukwama kujumuishwa kwenye makukbaliano ya Romelu Lukaku.

Baada ya klabu ya Chelsea kushinda kufanikisha usajiri wa Kounde sasa hivi wamehamisha nguvu zote kwa mlinzi huyo wa kati mwenye umri wa miaka 19 ili aweze kuziba nafasi ya ulinzi wa kati.

Chelsea wanaanda Offer ambayo kuikubali itakuwa mikononi mwa klabu ya Inter baada ya mazungumzo kuhusu Casadei kwani mpaka sasa klabu ya Inter milan haiko tayari kumpoteza mchezaji huyo

Casadei amekuwa sehemu ya makubaliano mbalimbali yaliofanyika kwenye majira haya ya kingazi, ingawa,  awali ilikuwa kwa ajiri ya uhamisho wa Lukaku na kwenye mazungumzo ya Gleison Bremer pia

Acha ujumbe