Nyota wa FC Barcelona, Philippe Coutinho, anatarajia kurejea Uingereza kwa mkataba wa mkopo kule Aston Villa.
Coutinho atarejea kwenye EPL kwa mara ya kwanza toka alipoondoka Liverpool na kwenda Barca. Maisha ndani ya LaLiga hayajaendana sana na uwezo wake anaojulikana nao. Lakini, yote 9, 10 ni muunganiko wa Philippe na Stevie G kwa mara ya nyingine.
Wawili hawa waliwahi kucheza pamoja kwenye safu ya kiungo pale Anfield na sasa, mmoja anakwenda kuwa mchezaji akiongozwa na swahiba wake ambaye sasa ni kocha mkuu.

Taarifa zinaripoti kuwa, Coutinho amefuzu vipimo vya afya nchini Ufaransa na sasa, anatarajiwa kutua Uingereza Jumanne kukamilisha taratibu za usajili kabla ya kuanza mazoezi rasmi na Aston Villa siku ya jumatano.
Huenda Philippe akawa miongoni mwa wachezaji watakaochuana na Manchester United kwenye mchezo wa EPL wikiendi hii pale Villa Park.
Ni muda wako kujiachia na mchezo maridhawa wa Almighty Aztec katika kasino bomba za meridianbettz. Nafasi ya kutengeneza mkwanja iko mikononi mwako kazi ni kwako.

CHEZA HAPA

