Klabu ya Tottenham Hotspur iko kwenye mazungumzo na klabu ya Wolves kwa ajiri ya kumsajiri winga wake Adama Traore ambapo wameweka kiasi cha £20 million ili kuweza kupata huduma.
Winga huyo mwenye umri wa miaka 25 anavutiwa na kuhamia katila klabu ya kaskazini mwa London na kocha wa klabu ya Tottenham Hotspur, Antonio Conte nae amepanga kukiimarisha kikosi chake mwezi huu.

Adama Traore amebakisha miezi 18 kwenye mkataba wake, na wolves wako tayari kumuweka sokoni baada ya kuona mchezaji huyo havutiwa tena kubaki kwenye kikosi hicho ili aweze kwenda sehemu ambapo atafurahi kuwepo.
Pia kuna tetesi kuwa klabu ya Barcelona nayo inavutiwa na huduma ya Traore, ikiwa Barcelona watakuwa kweli wanahitaji huduma yake wataleta ugumu kwenye mazungumzo yanayoendelea, lakini mpaka sasa hakuna offa yoyote rasmi iliyotumwa na Barcelona.
Tottenham hawako kwenye presha kubwa ya kuweza kuwaachia wachezaji wake kabla ya kusajiri wachezaji wapya, lakini pia kiasi chochote cha pesa kitakochopatika kwenye mauzo ya wachezaji msimu huu kitatumika kuimarisha kikosi kwenye dirisha hili la usajiri au majira ya kiangazi.
Ni muda wako kujiachia na mchezo maridhawa wa Almighty Aztec katika kasino bomba za meridianbettz. Nafasi ya kutengeneza mkwanja iko mikononi mwako kazi ni kwako.

CHEZA HAPA

