Klabu ya Chelsea imemtambulisha mchezaji wao mpya Wesley Fofana ambaye amaejiunga na Klabu hiyo akitokea Leicester City.

Beki huyo kitasa amejiunga na Chelsea kwa mkataba wa miaka sita (6), ambapo anaenda kuongeza nguvu kwenye kikosi cha Thomas Tuchel ambacho kimekuwa kinaupungufu kwenye baadhi ya maeneo ikiwemo eneo la ulinzi, baada ya Chelsea kumuuza beki wao kitasa Rudger kwenda Real Madrid.
Welcome, Wesley! 😁#FofanaIsChelsea
— Chelsea FC (@ChelseaFC) August 31, 2022
Chelsea na Leicester zilifikia makubaliano ya paundi 70M kama ada ya uhamisho ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa.
Klabu ya Chelesea tangu kuanza kwa msimu huu 2022/2023 wamecheza mechi 5, kashinda mechi 2 na kutoa sare 1, na kafungwa mechi mbili zote za ugenini.


