FIFA Wamfungia Maisha Refarii Fagla

Shirikisho la Soka Duniani, FIFA wamemfungia Kokou Hougnimon Fagla ambaye alikuwa ni refarii kujihusisha na soka kwa maisha yake yote baada ya kupatikana na hatia ya rushwa.

Kamati ya Maadili ya FIFA ilifungua uchunguzi mwezi machi mwaka jana baada ya Fagla ambaye alikuwa chini ya Shirikisho la Soka la nchini Togo kutuhumiwa kuwa alipokea rushwa kwaajili ya kupanga matokeo ya kirafiki ya kimataifa.

Kwa mujibu wa taarifa ni kuwa muamuzi huyu alishirikiana na Wilson Raj Perumal ambaye pia alikuwa anatuhumia kwa kupanga matokeo ya mechi za kimataifa kwa sababu shughuli za utabiri wa gemu hizo.

FIFA Wamfungia Maisha Refarii Fagla
Fagla (katikati) akitimiza wajibu wake.

Tamko la Shilikisho la Soka Duniani linasema kuwa Fagla alikiuka utaratibu na sheria za FIFA hivyo uamuzi uliuofikiwa ni kumfungia muamuzi huyu kwa maisha yake yote asijihusishe na soka.

3 Komentara

    Duuh..hatari

    Jibu

    Duh majanga

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.