Aliyekuwa meneja wa Manchester United kabla hajatimuliwa Jose Mourinho, sasa anasema yupo katika maandalizi ya kukipokea kibarua kingine cha umeneja katika msimu wa joto unaokuja.
Bwana huyu ambaye pia amewahi kuwa meneja wa klabu za Porto, Chelsea na Inter Milan ameshadaiwa kuzikataa ofa kadhaa zilizomfuata mapema kabisa baada ya kutimuliwa klabuni hapo.
Jose anasema yeye anaelewa nini anataka na nini hgataki, hivyo anajiandaa kuingia kibaruani msimu wa joto na anasubiri ofa nono zaidi ili aweze kwenda nayo sambamba. Mourinho baada ya kutimuliwa na United ameendelea kufurahia kujihusisha na soka kama mchambuzi katika vituo mbalimbali alivyokuwa akialikwa.
“Nitapendelea zaidi kurejea mwezi Juni, msimu wa joto mwanzoni kabisa mwa msimu. Ninafanya kazi, ninajiandaa kwa kazi nyingine msimu ujao”
Mourinho alikuwa akihusishwa na kurejea kule Real Madrid kabla klabu hiyo haijaamua kumrejesha Zinedine Zidane. Hata hivyo, ukiacha vibarua vinne anavyodaiwa kukataa, Jose anaripotiwa kuwa alikataa dili la kufundisha timu ya taifa pia.


Furahav
Namkubali sana hyu kocha morinho
Povel
Habar njema kwake