Marco Reus ni mfalme pale Signal Iduna Park , akilala akiamka bado ni mfalme watu wanakwenda wanapita wanamuacha pale . Ni kama mapenzi vile yaani kumvumilia mwenza wako katika hali yoyote , wengine wanasema mapenzi ya kweli yaliisha miaka ya 80 hakuna mapenzi saivi zaidi ya kusaidiana tu , hakuna mapenzi ya Agape saivi kila mtu anawaza faida yake . Penzi la Marco Reus na Borrusia Dortmund ni la Agape kila mtu anampenda mwenzake.

Marco Reus alianza katika timu za watoto za Borrusia Dortmund kabla ya kutimka kutafuta uzoefu Rot Weiss ahlen II na Borussia Monchengladbach aliwasha moto mkubwa na Dortmund kuamua kumrudisha nyumbani Signal Iduna Park . Mashabiki wa Borrusia wameweza kumpenda na wameshindwa kumchukia , amewaingia kwenye nyoyo zao na anawakosha , wakati Piere Aubemeyang anawaletea nyodo anataka kuhama wala hawakua na presha walijua Reus akitoka kitandani basi anakua boss . Mashikaji wake Roberto Lewandowski aliondoka yeye akabaki , aliondoka Shinji Kagawa , Mario Gotze , Nuri Sahin , Aubemeyang na mafundi wengine kibao lakini yeye hana huo muda , akitoka majeruhi wanamrudishia tambala la unahodha.
Miasha yake yametawaliwa na majeraha sio kila timu inauwezo wa kua na Marco Reus , Kizuri kwake akipona hahitaji muda mwingi kurudisha form yake anakupa kitu kizuri ambacho wachezaji timamu hawakupi . Muunganiko wake na Mario Gotze pale Dortmund enzi za Klopp ulisemekana ni hatari zaidii kwa kipindi kile. Kuelekea kombe la dunia 2014 pale Brazill alicheza mechi sita alifunga goli tano na assists tatu , ilibidi aondolewe katika timu itakayoshiriki kombe la dunia baada ya kuumia katika mechi ya kirafiki dhidi Armenia alilia sanaa..

Mashabiki wengi wa mpira waliaimini na wanaamini Reus hakutakiwa kuendelea kukaa pale Dortmund , katika ubora wake huwezi kumkataa kukaa kwake Bundersliga tena Dortmund sawa na kuishi gizani nani atamuona na kumzingatia ?? pengine ni bora ambavyo hakuondoka sababu hakuna uhakika wa moja kwa moja kwamba atang’aa pamoja na majeraha yake . Marco Reus ni kiungo mshambuliaji mwenye kasi kubwaa , uwezo wa kumilikia mpira ,uwezo mkubwa wa kufunga , anapiga kwa uzuri mpira iliyokufa na kikubwa anapiga mashuti makali mnooo.
Ameamua kuwatumikia BVB milele daima , hana dalili za kuondoka na inawezekana hafikirii , ameona kuna ufalme wake pale pamoja na swahiba wake Mario Gotze watoto wa kishua hawa . Wazazi wake waliamua kumpa jina la Marco ili kumuenzi legend wa soka wa Uholanzi Marco Van Basten , Reus ataendelea kua moja ya wachezaji bora kabisa katika kizazi chake alikua namba tatu katika wachezaji bora duniani mwaka 2013.


Theckla
Marco Reus ni kiungo mshambuliaji mwenye kasi kubwaa ssna
Ester mmakasa
Asante meridianbet kwa makala ya uwakika.
aisha
Marco reus yuko vizuri
Ernest
Reus ni mchezaji mwenye kijapi cha hali ya juu na ameisaidia sana Dortmund
Tahiya
Ni mchezaji mzur
Asha
Reus yupo vzr Sana ana nidhamu kubwa
mwakalosi
huyu reus atazeekea hapo
Mwanaidi
Nikiungo mpambanaji sana na ndio mana dortmund inamtegemea sana
Antony Luseno
Nakala nzuri #meridianbettz
Salma
Kiungo mzuri mwenye nidhamu& kujituma
Samiah
Nimchezaji mzuri sanaaa
Neema juma
Reus yuko vzr mno
Ester jackson
ameona kuna ufalme wake pale pamoja na swahiba wake Mario Gotze watoto wa kishua hawa
Elika
Hajakosea kwa hilo Reus yuko sawa kabisa
Agness
Nimchezaji maridadi
Hope mwaikuka
Namkubal sana
Adelta
Marco reus Yuko vizuri
felister
Reus ni mfalme watu wanakwenda wanapita wanamucha
Rehema
Mchezaji Yuko vizur
Khadija
duuh huyo bwana mdogo atazeekea hapo#meridianbettz
David Pere
Reus Ana kipaji na anajua mpira sanaa
Amani
Ni mchezaji mzuri pia Ni mpambanaji
winfrida
Mashabiki wa Borrusia wameweza kumpenda na wameshindwa kumchukia marco lous
Sadick
Reus amenikumbusha mapenzi aliyonayo Ramos kwa Real Madrid#meridianbettz
lombo
marco reus yuko poa sana
Gabriel
Huyo n kiungo mzur sana Dortmund
Caroline
Reus yupo vizuri..
Theonestina
Namkubar Sana Reus
Dorophina
Reus yupo vizuri sana
Asia Abdy
Kiungo hatar huyo
Emmy cleopa
Mchezaji mzur sana huyo
Hamidu
Talent player
Magdalena
Reus ni mchezaji mwenye kipaji Cha pekee na anatambua alifanyalo
Mariam mtandama
Mchezaji mzur