Meneja wa Atletico Madrid Diego Simeone amekanusha maneno kuwa wanamgwaya Lionel Messi wakiwa kwenye maandalizi ya kukutana uso kwa uso na mahasimu wao Jumamosi hii. “Hatumuogopi Messi… Valverde anafanya kazi bomba sana” haya ndiyo maneno ya meneja huyu akimsifia meneja wa Barcelona.
Kuuelekea gemu hii, Atletico Madrid wanatarajia kupata ushindi kwenye gemu hii ili kuendelea kuwa na matumaini ya kutwaa ubingwa. Barcelona wamewatupa Atletico nkwa pointi 8 zaidi, kitu ambacho kama Atletico watashindwa kupata pointi tatu safari yao ya matumaini itakuwa imefika tamati wakisubiri kumaliza msimu kwenye nafasi ya 2.
Messi amekuwa chachu ya ushindi uliopita wa Barcelona na ushindi wa gemu nyingi zingine klabuni hapo, anatambulika vyema kwa uwezo wake wa kubadili matokeo dakika za mwisho kabisa. Amekamilisha magoli 42 kwa gemu 39 alizocheza msimu huu, Lakini hajawa tishio kwa meneja wa Atletico ila wanamuheshimu.
Simione anasema Barcelona wanakuwa juu kwa sababu ya kazi nzuri ya meneja wao Valverde, wakiwa wanaweza kusimama vyema kwenye mashindano matatu. Simeone ameshindwa kupata ushindi kwenye gemu 14 za ligi akikutana na Barcelona kama meneja wa klabu hiyo. Wanahitaji kuandika historia mpya.
Omary lukumbi
Diego simione sio kama anamuogopa messi ila ana tengeneza kitu kitakacho zuia messi kupata mipira mara kwa mara ilikupunguza mashambulizi kutoka kwa.messi