Bernardo Silva Anakwenda Barcelona?

Kiungo nyota wa klabu ya Manchester City Bernardo Silva ameweka wazi nia yake ya kutaka kujiunga na klabu ya Barcelona msimu huu na tayari ameshafanya mazungumzo na wakala wake kuhusu swala hilo.

Klabu ya Barcelona imekuwa ikimfuatilia kwa muda mrefu mchezaji wa kimataifa kutoka nchini Ureno silva, na kwa sasa ananaoneka kuwa ndio mbadala sahihi ikiwa watamapomteza kiungo wao Frenkie de Jong, ambaye muda wowote kuanzia sasa anaweza kujiunga na Manchester United.

Bernardo Silva

Ijapokuwa, kwa sasa Bernardo Silva bado ana mkataba na klabu ya Manchester City ambao unatarajiwa kuisha mwaka 2025, lakini Pep Guardiola hana mpango wa kumuweka sokoni kwa sasa.

Bernardo Silva msimu huu ameichezea klabu ya Manchester City michezo 50 kwenye mashindano yote, huku akifanikiwa kufunga magoli 13. Pia Silva ametajwa kwenye kikosi cha ‘PFA Premier League Team of the Year’.


Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.