Zidane Anamtamani Mbappe, Watamsajili?

Zinedine Zidane amerejea klabuni Real Madrid siku kadhaa zilizopita baada klabu hiyo kuwa na wakati mgumu huu na kufanya maamuzi ya kumtimua aliyekuwa meneja wa klabu hiyo Santiago Solari. Zidane amerejea na anatamani kuwa kocha wa Mbappe!

Siku chache zimepita toka Real Madrid wathibitishe usajili wao wa kwanza klabuni hapoo baada ya kurejea kwa Zidane, ambao walimtaja staa wa FC Porto Eder Militao. Mbappe na Neymar pia wamekuwa wakihusishwa na mabingwa hawa wa Laliga.

Zidane alihojiwa kuhusu taarifa za klabu yake kuhusishwa na mastaa hao wawili na akawa anasita kuzungumzia suala hilo akisisitiza kuwa singependa kuzungumzia wachezaji ambao ni mali ya klabu nyingine. Lakikini pia akasema kiuhalisia angependa kuwa mwalimu wa Kylian Mbappe kama wachezaji wengine mashuhuri.

Real Madrid wanadaiwa kuwa wapo katika maandalizi ya kutumia mkwanja mrefu kwenye usajili unaokuja ili Zidane aweze kusuka upya kikosi chake tayari kwa kurejesha heshima, huenda staa huyu akawa kwenye orodha ya wachezaji wanaopangwa kunaswa na klabu hiyo.

Zidane Anamtamani Mbappe, Watamsajili?
“napenda kuwa mwalimu wa mbappe” -Zidane

3 Komentara

    Mchukue tu.

    Jibu

    Mchukueni tuu sio mbaya

    Jibu

    Habar njema sana 👍

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.