Jurgen Klopp Aitupialawama Ratiba-EPL.

Tangu kuanza kwa msimu huu, Jurgen Klopp ni miongoni mwa makocha wanoitupia lawama EPL kwa upangaji wa ratiba hasa kwa timu zinazocheza mashindano mengi.

Turudi nyuma kidogo, Manchester United walitoka kucheza nchini Uturuki (Jumatano) na timu ya Istanbul Basaksehir ambapo walipoteza kwa kufungwa 2-1 na walitakiwa kucheza na Everton siku ya Jumamosi mchana.

Kitu hicho hicho kinatokea kwa Liverpool wiki hii, baada ya kucheza jana kwenye Ligi ya Mabingwa dhidi ya Atalanta, watasafiri kuwafata Brighton Albion jumamosi mchana. Ni siku 2 tu za kupumzika na kujiandaa na mchezo huu.

Upangaji huu wa ratiba ni kati ya vitu ambavyo Jurgen Klopp anavilaani kwani vinawaumiza wachezaji kwa kiasi kikubwa.

Jurgen Klopp ameiambia BT Sports kuwa ” ninaogopa kusema lakini ninadhani haitotokea kwetu tu bali na kwa timu zingine pia.

“Unatupanga sisi kucheza Jumamosi saa 9:30 mchana, huo ni uhalifu kusema ukweli. Hiyo haihusiani chochote na mchezo wetu wa leo usiku (dhidi ya Atalanta).

“Ninachoshukuru kwa sasa ni kwamba sijapata majeruhi wengine. Kwa sasa tunatakiwa kuwa fit haraka sana. Wachezaji hawajafurahia matokeo lakini hatuna muda na hilo kwa kweli.

“Ni suala la kujiandaa upya na kuendelea mbele.”

Kipigo cha Liverpool kinawafanya waendelee na mchakato wa kuisaka nafasi ya kufuzu hatua ya 16 bora kwenye Ligi ya Mabingwa, wanahitaji ushindi katika mechi 1 tu kati ya 2 walizobakiwa nazo ili wafuzu kwenye hatua hiyo.


USICHELEWE KUKAMATA MKWANJA HUU!

Hadi 130,000,000 TSH Kutolewa kwa washiriki wa shindano la Playson Cashfall. Unaipata kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet Pekee. Jisajili sasa, kisha ingia mchezoni kabla ya Novemba 29.

Meridianbet Tanzania Casino

SOMA ZAIDI

20 Komentara

    Ratiba mbona iko sawa tu

    Jibu

    Namuunga mkono kloppa ratiba mbaya ndio mana hata matokeo yake mabovu kwa timu nyingi

    Jibu

    Kloop yupo sahii kwaalicho kiongea anajua yeye ajakaa sawa kwasababu matokeo mabovu

    Jibu

    Ratiba ipo poa sana

    Jibu

    lawama hazitosaidia chochote yeye akubaliane na matakwa ya epl tu

    Jibu

    Ratiba ipo vizuri

    Jibu

    Ratiba tumeielewa

    Jibu

    Ratiba iko poa sana sema tu hawajajipanga

    Jibu

    Ratiba ipo sawa

    Jibu

    Iko poa ratiba

    Jibu

    Kloop nae aache lawama

    Jibu

    Ratiba imekaa poa hiyo

    Jibu

    Lamama za nn sasa

    Jibu

    Kuna kitu hakipo sawa

    Jibu

    Ratib iko powah sana

    Jibu

    Imetulia sana hii ratiba

    Jibu

    Good news

    Jibu

    Nic

    Jibu

    Ratiba nzuri

    Jibu

    Ni kweli imechangia sana wachezaji kuwa majeruhi

    Jibu

Acha ujumbe