Tangu kuanza kwa msimu huu, Jurgen Klopp ni miongoni mwa makocha wanoitupia lawama EPL kwa upangaji wa ratiba hasa kwa timu zinazocheza mashindano mengi.
Turudi nyuma kidogo, Manchester United walitoka kucheza nchini Uturuki (Jumatano) na timu ya Istanbul Basaksehir ambapo walipoteza kwa kufungwa 2-1 na walitakiwa kucheza na Everton siku ya Jumamosi mchana.
Kitu hicho hicho kinatokea kwa Liverpool wiki hii, baada ya kucheza jana kwenye Ligi ya Mabingwa dhidi ya Atalanta, watasafiri kuwafata Brighton Albion jumamosi mchana. Ni siku 2 tu za kupumzika na kujiandaa na mchezo huu.
Upangaji huu wa ratiba ni kati ya vitu ambavyo Jurgen Klopp anavilaani kwani vinawaumiza wachezaji kwa kiasi kikubwa.
Jurgen Klopp ameiambia BT Sports kuwa ” ninaogopa kusema lakini ninadhani haitotokea kwetu tu bali na kwa timu zingine pia.
“Unatupanga sisi kucheza Jumamosi saa 9:30 mchana, huo ni uhalifu kusema ukweli. Hiyo haihusiani chochote na mchezo wetu wa leo usiku (dhidi ya Atalanta).
“Ninachoshukuru kwa sasa ni kwamba sijapata majeruhi wengine. Kwa sasa tunatakiwa kuwa fit haraka sana. Wachezaji hawajafurahia matokeo lakini hatuna muda na hilo kwa kweli.
“Ni suala la kujiandaa upya na kuendelea mbele.”
Kipigo cha Liverpool kinawafanya waendelee na mchakato wa kuisaka nafasi ya kufuzu hatua ya 16 bora kwenye Ligi ya Mabingwa, wanahitaji ushindi katika mechi 1 tu kati ya 2 walizobakiwa nazo ili wafuzu kwenye hatua hiyo.
Hadi 130,000,000 TSH Kutolewa kwa washiriki wa shindano la Playson Cashfall. Unaipata kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet Pekee. Jisajili sasa, kisha ingia mchezoni kabla ya Novemba 29.
Nasra
Ratiba mbona iko sawa tu
Ester jackson
Namuunga mkono kloppa ratiba mbaya ndio mana hata matokeo yake mabovu kwa timu nyingi
Lydia Emmanuel Magoti
Kloop yupo sahii kwaalicho kiongea anajua yeye ajakaa sawa kwasababu matokeo mabovu
Khadija
Ratiba ipo poa sana
magdalena
lawama hazitosaidia chochote yeye akubaliane na matakwa ya epl tu
Saupha mohamed
Ratiba ipo vizuri
Adelta
Ratiba tumeielewa
Dorophina
Ratiba iko poa sana sema tu hawajajipanga
Tatu
Ratiba ipo sawa
Sarah
Iko poa ratiba
aisha
Kloop nae aache lawama
Genia Sikaluzwe
Ratiba imekaa poa hiyo
Hopemwaikuka
Lamama za nn sasa
Caroline
Kuna kitu hakipo sawa
Fatina mfingi
Ratib iko powah sana
samiah
Imetulia sana hii ratiba
Tahiya
Good news
Rahma
Nic
Sauda
Ratiba nzuri
warda
Ni kweli imechangia sana wachezaji kuwa majeruhi