Baada ya harakati za kutaka kuondoka Barcelona kutozaa matunda. Lionel Messi atamka hadharani matamanio yake ya kucheza Ligi Soka nchini Marekani – MLS.
Lionel Messi aliutikisa ulimwengu wa soka baada ya kuwasilisha ombi la kuondoka Barcelona mwezi Augosti. Licha ya kwamba ombi lake halikufanikiwa, Messi anaendelea kuitumikia klabu hiyo mpaka mwishoni mwa msimu huu mkataba wake utakapoisha.
Messi amekuwa akihusishwa na vilabu mbalimbali kama vile Man City na PSG lakini kugusia suala la kucheza Marekani, pengine litaibua picha nyingine.
Akizungumza na kituo cha televisheni cha La Sexta nchini Hispania, Lionel Messi amesema “bado sijajua nitafanya nini.
“Nitasubiri mpaka mwishoni mwa msimu. Ningependa kwenda kucheza Marekani na kujifunza maisha na ligi ya kule lakini nitarudi Barcelona kwa kiasi fulani.
“Kwa sasa ninaiangalia zaidi Barcelona na kumaliza msimu huu vizuri, lengo ni kushinda mataji na sio kuyumbishwa na mambo mengine.”
Msimu uliopita, Barcelona hawakubeba taji lolote na wanashikilia nafasi ya 5 kwenye msimamo wa La Liga msimu huu. Huu ni mwanzo mbaya kwa miamba ya Catalunya na ni historia baada ya miaka 33.
VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!
Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini???
Chiku
Wako juu
Shakila mrope
Kipajai anacho ana haki ya kuchezea timu yeyote ile duniani
Sarah
Yuko vizuri lazima atambe
Tatu
Itakuwa vizuri mess akiahama Barcelona
Mwanahamisi
Yuko vizuri
Dorophina
Messi akitaka kwenda kokote hakuna sehemu watamkataa kutokana na uwezo wake
Rahmal
Yuko poa
Hopemwaikuka
Sio mbaya kubadlisha mazingra
Adelta
Messi Yuko vizuri na anakubalika
Angelina
Messi atulie tu barcelona
Lydia Emmanuel Magoti
Messi anaweza kuongea kitu chochote kwasababu yeye nimchezaji anae jiamini
Issa
Saf kwake
warda
Atacheza tu ni swala la mda