Real Madrid wanakutana na Granada leo, na Marcelo atakuwepo nje ya dimba akiripotiwa kupishana kauli na meneja wake Zinedine Zidane.
Kwa mujiu wa chapisho la Mail Online beki huyu ametofautiana na Zidane kwenye suala la mbinu za meneja huyo na upangaji wake wa kikosi.
Taarifa zinaonesha kuwa moja ya sababu ambayo imesababisha mgongano kati ya wawili hao ni juu ya mda wa mechi wa beki huyu wa kati, ambaye analalamikia kuwa na wakati mchache, huku akikosa imani na mbinu na uchaguzi.
Marcelo ameendelea kuwa na mda mchache wa kucheza klabuni hapo, Ferland Mendy akipewa kipaumbele zaidi yake. Kwa mujibu wa Goal, Suala hili limekuwa kubwa kiasi cha kuleta sura tofauti kuelekea mechi dhidi ya Granada, na imechochea maamuzi ya Zidane kumweka Benchi Marcelo.
Wakati Mendy akiripotiwa kuwa angekuwa nje kwa sehemu yote ya msimu iliyosalia, staa huyo alidhani huu ulikuwa wakati wake muafaka wa kutetea nafasi yake, mpaka hali ilipoonekana kuwa tofauti.
Marcelo amekuwepo na Real Madrid tangia mwaka 2007 na amecheza zaidi ya mechi 370.
Hii ndiyo burudani yenye ushindi! Ingia kwenye kasino ya Meridianbet kufukuzia ushindi huu. Cheza sasa Lucky Lucky na uwe moja ya washindi na Mabingwa.
aisha
Wayamalize yaishe ili kusudi kazi iendelee
Issa
Marcelo tundika daruga
Johnmary jo
Wasameheane na kazi iendelee hakuna mtu ambaye akosei kwa mwenzake
Venerose
Waombane radhi tu
Adelta
Wakae chini waelewane tu maisha yaendee
Theonestina
Duuuh
Lydia Emmanuel Magoti
Duuh
Elika
Kazi mbele