Staa Neymar wa Paris Saint-Germain amesema anataka kucheza na Christiano Ronaldo hali ya kuwa kumekuwa na uvumi wa Ronaldo kuondoka Juventus na kutua PSG.
Ronaldo, ambaye alifikisha mabao 100 kwa Juventus wakati wa ushindi wa 3-1 siku ya Jumatano huko Sassuolo, ametajwa kuwaacha miamba wa Serie A mwishoni mwa msimu.
Mshindi huyo mara tano wa Ballon d’Or amehusishwa na Paris Saint-Germain, na vilabu vya zamani vya Manchester United na Real Madrid.
Nyota wa PSG Neymar – ambaye amesaini kandarasi mpya na watetezi wa Ligue 1 – alizungumza juu ya ushirikiano na Ronaldo, baada ya kucheza pamoja na Lionel Messi wa Barcelona.
“Nataka kucheza na Cristiano Ronaldo,” mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazil mwenye umri wa miaka 29 aliiambia GQ.
“Tayari nimecheza na wachezaji bora, kama [Lionel] Messi na [Kylian] Mbappe, lakini bado sijacheza na Cristiano Ronaldo.”
Neymar amesainiwa na PSG hadi 2025 kufuatia mpango wake mpya katika mji mkuu wa Ufaransa.
Mshambuliaji huyo alijiunga na mabingwa wa Ligue 1 kutoka Barcelona kwa mkataba wa miaka mitano kwa gharama ya rekodi ya dunia ya € 222milioni mwezi Agosti 2017.
Hii ndiyo burudani yenye ushindi! Ingia kwenye kasino ya Meridianbet kufukuzia ushindi huu. Cheza sasa Lucky Lucky na uwe moja ya washindi na Mabingwa.
Utaweza ? au ndio maneno tuu
Itakua poa
Nimawazo mazuri sanaa viongozi pamoja na wahusika wakae pamoja waone watakuja VP ili waweze kucheza pamoja
Itakuwa safi sana
Itakuwa vizuri Sana
Mawazo manzur
Itakua vizuriii
Itakuwa poa tu
Itakuwa poa