Nyota wa Barcelona, Pedri atashindwa kuwa sehemu ya mechi ya Jumatano ya Copa del Rey kwenye hatua ya nusu fainali dhidi ya Sevilla.
Kinda huyu wa miaka 18, ambaye amekuwa sehemu ya msingi ya kikosi cha Koeman msimu huu alilazimika kutoka nje baada ya kupata jeraha kwenye mechi ya Laliga dhidi ya kikosi cha Julen Loptegui Jumamosi.
Nafasi ya Pedri ilichukuliwa na kinda mwenzake Ilaix Moriba kwenye dakika 71 zilizosalia, na Barcelona wamethibitisha kuwa kinda huyo hataweza kucheza tena mechi inayofuata kutokana na hali aliyonayo sasa.
Klabu haijabainisha mda rasmi ambao staa huyu hatapatikana uwanjani lakini wamethibitisha kuwa ataikosa mechi dhidi ya Sevilla Jumamosi.
Kiungo huyu anaungana na wenzake wengine kama Ansu Fati, Philippe Coutinho na Sergi Roberto ambao pia hawatashiriki mechi ijayo, hata hivyo kuna uwezekano kuwa akaimarika na kushiriki vyema kwenye mechi zilizozalia za Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Ni Muda wa Kuvuna Mkwanja na Jungle Jim and the Lost Sphinx
Hauihitaji kufikira mara mbili ni mchezo gani utakupatia mkwanja ndani ya kasino za Meridianbet. Jiunge sasa ufurahie Jungle Jim and the Lost Sphinx.
Pedri pole sana
Dogo majeraha yanamwandama sana
Duu pole yake
Get well soon Pedri
Pole
Pole yake
Pole yake
Pengo barca
Sorry for him