Mshambuliaji wa Wolves, Pedro Neto anatarajiwa kuwa nje ya mpaka mwisho wa msimu kutokana na majeraha ya goti aliyoyapata kwenye mechi dhidi ya Fulham.
“Neto alipata majeraha ya kifundo cha goti wakati wa mechi na Fulham” ilieleza taarifa ya Wolves.
Pedro amecheza mara 35 akiwa na Wolves msimu huu, huku akifunga magoli matano na kutoa pasi za magoli tano.
Wolves pia wataendelea kukosa huduma ya beki wao Johny na Marcal ambao bado wapo majeruhi. Huku kiungo wao Reuben Neves akipimwa kuwa na maambukizi ya Covid-19 kwahiyo atakuwa nje ya kikosi kwa muda.
Wolves hawajakuwa na mwenendo mzuri sana wa uchezaji wao huku ikiwa na alama 38 kati nafasi ya 12. Wakishinda mechi 10 na kupoteza 13.
Wolves watacheza na Sheffield United jumamosi hii bila ya nyota wao hao wanne.
Kila mtu ana namba zake za bahati, Meridianbet tunatambua namba zinaweza kukufanya milionea leo. Jilipe kwa namba zako za bahati kila baada ya dakika tano.
dorophina
Pole yake pedro
Sarah
Pole yake pedro
Venerose
Pole sana Pedro
Angelina
Pole yake
Hopemwaikuka
Ugua pole
warda
Pole yake