Mshambuliaji wa klabu ya Manchester United Marcus Rashford amefanikiwa kuchukua tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Disemba ndani ya klabu ya Man United.
Mshambuliaji huyo ameshinda tuzo hiyo akiwashinda wachezaji wenzake wawili ambao ni beki Luke Shaw pamoja na kiungo wa shoka Carlos Casemiro. Mashabiki wa klabu ya Man United ndio wamefanikiwa kumpa tuzo hiyo Rashford baada ya kuonekana mchezaji huyo ndio ameongoza kwa kupigiwa kura.
Mshambuliaji huyo amekua kwenye kiwango bora sana msimu hasa baada ya kurejea kwa ligi baada ya mapumziko ya kombe la dunia mwezi Disemba. Mchezaji huyo amekua msaada mkubwa sana ndani ya klabu ya Manchester United kutokana na mabao ambayo amekua akifunga.
Mshambuliaji Marcus Rashford amefanikiwa kufunga mabao jhusika kwenye mabao manne ndani ya mwezi Disemba akifanikiw akufunga mabao matatu na kupiga pasi moja ya bao, Mchezaji huyo amekua na ubora mkubwa sana kwenye siku za hivi karibuni.
Mshambuliaji Marcus Rashford ameonekana kuboresha kiwango chake mara dufu msimu huu kwani mpaka sasa amehusika kwenye mabao 21 kwenye michezo 27, Huku msimu uliomalizika akiwa amefunga mabao matano ndani ya msimu mzima.

