Mshambuliaji mpya wa klabu ya Manchester United Wout Weghorst atakuwepo kwenye kikosi cha klabu hiyo kitakachosafiri kwenda kuwavaa klabu ya Crystal Palace.
Klabu ya Manchester United itasafiri hadi jijini London kwenda kumenyana na klabu ya Crystal Palace siku ya jumatano katika mchezo wa ligi kuu ya Uingereza ambapo inaelezwa mchezaji Wout Weghorst atakua kwenye kikosi cha klabu hiyo kitachoivaa Palace.
Mshambuliaji Wout Weghorst ambaye amejiunga na klabu hiyo kwenye dirisha la usajili mwezi huu wa Januari akitokea klabu ya Besiktas ya nchini Uturuki, Huku akipewa nafasi ya kufanya vizuri ndani ya klabu hiyo kutokana na imai ya kocha wa klabu hiyo aliyoiweka kwake.
Mshambuliaji huyo watu wengi wanatarajia afanye vizuri ndani ya klabu hiyo kama ambavyo amewahi kufanya mshambuliaji mwenzake raia wa Uholanzi Ruud Van Nistelrooy. Nistelrooy amewahi kufanya vizuri ndani ya klabu ya Manchester United miaka iliyopita.
Wout Weghorst hatizamiwi kuanza katika mchezo kati ya Manchester United dhidi ya Crystal Palace, Lakini mchezaji huyo atakuepo sehemu ya kikosi ambacho kitakachosafiri mpaka jijini la London suala la kucheza kwenye mchezo huo lipo chini ya mwalimu Erik Ten Hag.

