Kagera Sugar Bado Inajipanga!

Baada ya kuwa na mwenendo usioridhisha, Uongozi wa Kagera Sugar umeweka wazi kuwa, kikosi kwa sasa kitabaki Jijini Mwanza kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wao dhidi ya Singida Big Stars .

Mchezo huo wa raundi ya tano inatarajiwa kupigwa Septemba 27 katika uwanja wa CCM Kirumba Mwanza.

Ofisa Habari wa kagera Sugar, Hamis Mzanzala amesema: “Kikosi kinaendelea vizuri japokuwa mchezaji wetu Deogratius Mafie anaendelea na matibabu baada ya kupata majeraha mazoezini kabla ya kuanza Kwa Ligi Kuu hivyo alilazimika kwenda kufanyiwa upasuaji nchini Afrika Kusini.

“Tutaendelea kubaki Jijini Mwanza, kwaajili ya maandalizi ya mchezo wetu dhidi ya Singida Big Stars.

“Kocha wetu Mkuu, Francis Baraza pamoja na benchi lake la ufundi wanaendelea kufanya maboresho yote ya mapungufu na makosa yaliyojitokeza kwenye mchezo wetu uliopita, ili tufanikiwe kufanya vizuri na kupata alama tatu mbele ya Singida.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.