Kaze: Tuisapoti Timu Kwenye Kipindi Kigumu

Kocha Msaidizi wa Yanga, Cedric Kaze amewataka mashabiki wa timu hiyo kuwapa sapoti wachezaji na benchi la ufundi hata katika kipindi kigumu.

Kaze amezungumza hayo baada ya timu hiyo kufanikiwa kuvuka katika hatua ya makundi ya michuano ya Shirikisho barani Afrika.

Kaze alisema kuwa: “Niliongea baada ya mchezo wa kwanza kumalizika Dar kuwa tuna dakika 90 nyingine ugenini lakini watu walijua tunatolewa.

“Tuliwaona kwenye mchezo wa nyumbani walikuja na mbinu ya kuzuia tu na tulijua katika mchezo wa marudiano watakuja kwa lengo la kushambulia hivyo sisi tulikuja na mpango wetu.

“Tunawaomba wapenzi na mashabiki wetu wawe na timu tukiwa kwenye wakati mgumu kwa ajili ya kutusapoti.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.