Klabu ya Tottenham Hotspur inaripotiwa kuwa mbioni kumfuta kazi kocha wa muda, Igor Tudor, kufuatia kipigo cha aibu cha mabao 3-0 nyumbani dhidi ya Nottingham Forest. Matokeo hayo yamewaacha Spurs wakiwa nafasi ya 17 kwenye msimamo wa ligi, pointi moja tu juu ya mstari wa kushuka daraja.

Hali ya mambo ndani ya klabu imebadilika haraka kutoka kwenye matumaini ya kufanya vizuri hadi presha kubwa ya kuondolewa ligi kuu kutokana na msimamo wa ligi kwa sasa, huku uongozi ukiona mapumziko ya kimataifa kama nafasi sahihi ya kufanya mabadiliko. Licha ya sare dhidi ya Liverpool FC na ushindi dhidi ya Atletico Madrid, kipigo hicho cha karibuni kimeonekana kuwa pigo la mwisho kwa Tudor.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Tangu ateuliwe, Tudor ameshinda mechi moja tu kati ya saba, akipata sare moja na kupoteza tano huku timu yake ikiruhusu mabao 20. Takwimu hizi mbaya zimeifanya bodi ya klabu kuanza harakati za haraka za kutafuta kocha mpya kabla ya msimu haujaenda mbali zaidi.
Miongoni mwa majina yanayotajwa kuchukua nafasi hiyo ni Roberto De Zerbi, ambaye anaonekana kuwa chaguo kuu kutokana na uzoefu wake kwenye Ligi Kuu England. Pia, makocha wa zamani kama Harry Redknapp na Glenn Hoddle wanatajwa kama chaguo la muda mfupi kujaribu kuiokoa timu.

Hata hivyo, changamoto kubwa kwa Tottenham ni kumshawishi kocha wa kiwango cha juu kujiunga nao katikati ya msimu huku timu ikiwa kwenye hatari ya kushuka daraja. Mechi zijazo zitakuwa za maamuzi, na yeyote atakayechukua nafasi hiyo atalazimika kuleta matokeo ya haraka ili kuzuia msimu huu kugeuka kuwa janga kubwa kwa Spurs.

