Mike Tyson Atawezana Akirejea Ulingoni?

Sote tunafahamu bondia Mike Tyson aliamua kustaafu rasmi mwaka 2005. Tangia hapo bingwa huyu hajapigana ndondi za kulipwa mpaka sasa. Lakini Tyson anataka sasa kurejea Ulingoni.

Licha ya kustaafu, Mike Tyson aliendelea kupeta kwenye tasnia ya filamu akishirikiana na waigizaji wengi wakubwa duniani. Hivi karibuni akiweka wazi nia yake ya kurejea ulingoni amesema tayari anafanya mazoezi kujiweka fiti.

Mike Tyson amekuwa akifanya mazoezi hayo kuelekea shindano linaloweza kuandaliwa kwa ajili ya maonesho ya ndondi ili kukusanya pesa za kusaidia jamii.

Bondia huyu mwenye miaka 53 sasa, ana rekodi ya matumizi ya madawa, usumbufu wa kutumia madawa ulitua kwa nyota huyu.

Akizungumza na TI kupitia ukurasa wake wa Instagram, alisema kuwa anajinoa vilivyo kurejea

“Mwili wangu umechangamka sana, na maumivu ya kupiga mitt. Nimekuwa nikifanya mazoezi, nimekuwa nikijaribu kutafuta maonesho ya ndondi. Nitarejea kwenye fomu na nitaweza kupigana kama raundi 3 au 4 kwa ajili ya kukusanya pesa za msaada” -Mike Tyson

Mike Tyson
Mike Tyson katika pambano dhidi ya McBride 2005

Mike Tyson aliaamua kustaafu baada ya kupambana dhidi ya Kevin McBride na kushindwa kuendelea katika raundi na raundi ya 7 licha ya kuongoza kwa pointi hadi raudni ya 6. Aliona ulikuwa ni wakati muafaka yeye kustaafu baada ya kutawala ndondi kwa mda mrefu.

4 Komentara

    Mike Tyson is one of the greatest

    Jibu

    He is the one of the boxing legend

    Jibu

    Bingwa wa dunia.

    Jibu

    Dunia mzima inamtambuwa
    Tumpe hongera zake

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.