De Bruyne Ndio Kiungo Bora Duniani Kwa Sasa - Guardiola.

De Bruyne aliipatia City goli la penati kwenye mchezo dhidi ya Liverpool dakika ya 25 baada ya Joe Gomez kumchezea madhambi Raheem Sterling,ambaye alifunga timu yake hiyo ya zamani  goli la pili baada ya dakika kumi kupita.

Phil Foden aliweka kambani goli la tatu kabla ya Alex Oxlade-Chamberlain kujifuga goli la nne alipo jaribu kuzuia shuti la Sterling na kufanya Liverpool kulala kwa goli 4-0.

De bruyne alihusika kwenye magoli mawili na kiwango alichokionesha katika mchezo huo kimemfanya mwalimu wake Guardiola aweze kumtaja kama ndio kiungo wa kati bora kwa sasa ulimwenguni.

“Ni mchezaji mzuri sana, anakitu cha pekee katika soka lake,” Guardiola aliwaambia waandishi baada ya mchezo kumalizika.

“Anaweza akakimbia na kufungua macho yake kuangalia wachezaji wenzake, kiwango anacho kionesha kwa sasani kikubwa amefunga penati nne mfululizo kwenye nechi tulizo cheza.

“Kwa sasa katika nafsi ya kiungo ni bora kabisa.

“Ni kweli anaweza akawa bora zaidi. kivipi? Yeye anajua.”

Foden kwa mara nyigine ameweza kuwa na mchango mzuri katika mchezo huu, akiwa na timu ya Uingereza ya vijana wenye umri chini ya miaka 21 kiungo huyo amejihakikishia goli la nne katika michezo mitatu ya Premier League  tangu ligi irejee.

“Tuna jitahidi kumlinda,” alisema Guardiola.

“Hatumchezeshi kila mechi, kwa wachezaji wadogo ni kuwa na umakini nao katika hatua za mwanzo.

“Ni mchezaji wa aina yake anafanya vitu ambavyo vinanishawishi kusema kwamba kwa siku za mbele atakua mchezaji wa kiwango cha juu sana.

Mchezaji mwenzake waliomaliza pamoja kwenye Academy Eric Garcia alirudi dimbani baada ya kupona maumivu aliyoyapta kwenye mchezo dhidi ya Arsenal ambapo City walishida kwa 3-0 na mchezo dhidi ya Liverpool alianza kama beki wakati.

“Amecheza dhidi ya Salah na Mane na ana umri wa miaka 19 tuu, alikuwepo kwenye mazoezi kwa siku tatu au nne baada ya kukaa nje kwa siku kumi na alicheza vizuri sana.


Eric Garcia na Phil Foden

“Kama timu tunajivunia kuwa na hawa vijana Phil na Eric tunawahesabu katika kikosi bila shaka.”

 

46 Komentara

    Vizur

    Jibu

    Guardiola yupo sahihi Kevin ameisaidia sana man city

    Jibu

    KDB ni kiungo bora kwa sasa ,hilo halina ubishi. Huwa najiuliza kwanini Chelsea ya Mourinho haikuona hilo#meridianbettz

    Jibu

    Anachokisema guardiola ni Cha kweli kabisa

    Jibu

    Ni mchezaji mzuri sana ana kitu cha pekee kwny soka lake

    Jibu

    Pongezi sana timu ya Manchester city kwa kuonyesha mko vizuri mkizingatia mlikuwa na majeruhi lakini kijana mdogoahiri na matata Kevin De Bruyne aliweza kutamba sana uwashani na kuwashinda mabigwa wa Liverpool kwa magoli 4-0 mpaka ikampelekea mwalimu Guardiola aweze kumtaja kama ndio kiungo wa kati bora kwa sasa ulimwenguni inafurahisha sana kwa kweli .#meridianbettz

    Jibu

    De bruyne ni kiungo mzuri Sana pia hameisaidia timu ya Manchester city kwa kiwango kikubwa Sana timu yake ni mchezaji mzuri Sana pia hata kweny timu yake ya taifa ya ubeligiji Yuko vizuri gardiola hajaongopa kabisah

    Jibu

    Kweli kabisa

    Jibu

    Guardiola ni kiungo Bora anaejitabuwa na yupo sahihi

    Jibu

    Yah nivizuri akitoa kitu alicho kuwanacho moyoni kukipongeza nakukisifia Guardiola yupo sahii kuongea

    Jibu

    De bruyne ni mchezaji mzuri sana anakiatu cha kipekee katika soka lake la mpira pia hana mchango mkubwa sana man city kwa uwezo wake alio ufanya hanastairi pongezi sana

    Jibu

    Ni sahihi kabisa

    Jibu

    Ni mchezaji mzuri sana, anakitu cha pekee katika soka lake

    Jibu

    Lazima aseme hivyo kwa sababu nimchezaji wake

    Jibu

    Kocha Guardiola anachosema yupo sahihi kabisa mchezaji wake sio wa mchezo mchezo mpambanaji na anajua anachokifanya

    Jibu

    Hilo halina ubishi japo ni mchezaji asiyezungumziwa sana

    Jibu

    hayo n maon yake

    Jibu

    Tarent plaper#meridianbettz

    Jibu

    Ni mchezaji wa aina yake anafanya vitu ambavyo vinanishawishi kusema kwamba kwa siku za mbele atakua mchezaji wa kiwango cha juu sana.

    Jibu

    Yaaan lazima aongee hivo kwa sababu ni mchezaji wake#meridianbettz

    Jibu

    Ninamkubali sana#meridianbett

    Jibu

    De Bruyne sio kiungo bora tu duniani kwa sasa bali ni kiungo bora duniani anaeishi,uchezaji wake wa mpira ni moja kati ya viungo bora waliowahi kutokea duniani

    Jibu

    Kiwango cha De brunye kwa sasa kipo juu na anajua kutawala sana kiungo ingawaje majeruhi yamekuwa yakimuandama hapo nyuma na kufanya city kuteteleka kidogo ila anaimudu nafasi na atakuwa bora sana
    Kwa mbeleni

    Jibu

    Habar njema sana 👍 kwa mkongwe huyo japo kashazeeka ila waswahil tunasema anazeeka vzur

    Jibu

    De brune ni mchezaji mzuri Sana hakuna asiyefahamu ilo kikubwa kwa msimu huu kilicho muangusha kupafomu vizuri ni majeraha ya Mara kwa Mara ila ni bonge la player

    Jibu

    Jamaa yupo poa licha ya pepe gardiola kuona kuwa de bruyne ni kiungo bora duniani jamaa anajituma na uchezaji wake ni wakipewa unaweza kumuweka popote na klabu yeyote akakupa matoke uchezaji wake anaweza cheza liverpool,buyern munich,real madrid na PSG kwa staili anayochezea me namfananisha na viungo ambao waliopita kama Paul school,frank lampard,Steven gerradi na alonso.de brunyne anacheza popote

    Jibu

    Ligi ikianza Tena Mambo yatakuwa matamu kinyama#Meridianbetz

    Jibu

    De Bruyne fundi sana

    Jibu

    Safii

    Jibu

    Nlkua cjui hii

    Jibu

    Nimtazamo wake

    Jibu

    Nisawa kbs

    Jibu

    Big up

    Jibu

    Hongera brune.

    Jibu

    Ni mchezaji mzuri

    Jibu

    Kweli kabsaa

    Jibu

    Kelvin de bruyne sio mbaya n fundi wa kibeljiam mzungu chuma ila sio top Middlefielder kuliko wote dunian ila kwa maoni ya pep yeye yuko sawa kwa upande wake

    Jibu

    Kwa maoni yake yeye

    Jibu

    Hakika ni kiungo Bora anayejitambua

    Jibu

    KDB ni kiungo bora kwa sasa ,hilo halina ubishi.

    Jibu

    Ni sahihi kabisa

    Jibu

    Kvd yupo vzr lkn tuwape muda wa kuwa vzr Zaid hv Sasa nmapema Sana kusema kafika ubora wa viungo waliopitah

    Jibu

    Maoni yake km Koch huwez mkataz ila kwang kuna walio mzd

    Jibu

    Asante sana

    Jibu

    Maoni:De Bruyne yuko vizuri

    Jibu

    Guardiola yuko sahihi kabisa

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.