Coutinho: Arsenal Wapewa Nafasi

Kufuatia usajili wa moja kwa moja wa Philippe Coutinho kuendelea kubaki Bayern Munich kukwama. Sasa Barcelona wanatafuta suluhisho la mchezaji huyo ambaye anaonekana hana namba katika kikosi chao kwa sasa.

Vilabu mbalimbali vimekuwa vikihusishwa na usajili wa Coutinho kwa siku za hivi karibuni. Chelsea, Man United, Totenham na Arsenal ni kati ya vilabu vinavyotajwa kuisaka saini ya mbrazili huyo.

 

Taarifa zilizopo kwa sasa ni kwamba Arsenal na Totenham ndio timu zilizobaki katika kuwania saini ya Coutinho ambaye pia anaona nafasi ya kurudi tena kunako Ligi Kuu Uingereza – EPL baada ya kuiacha Liverpool miaka kadhaa iliyopita, ni fursa ya kipee kwake.

Inasemekana Arsenal wamejipanga kumtoa kiungo wao Matteo Guendouzi na kiasi cha fedha takribani pauni milioni 9 ili kumsajili Coutinho.Ofa hii inaonekana itasaidia pande zote mbili – Arsenal na Barcelona ambao wachezaji hawa wanaonekana kutokuwa kwenye mipango ya muda mrefu ya vikosi hivi.

Uongozi wa Arsenal unasubiri kuiona hatma ya Arsenal katika fainali ya Kombe la FA watapokutana na Chelsea. Endapo Arsenal watafanikiwa kunyanyua kombe hilo, watakuwa katika nafasi nzuri kiuchumi na hivyo bajeti ya usajili itaongezeka kwa kiasi fulani.

Arteta bado anakuwa mwenye mashaka katika hili kwani Juventus nao wanaonekana kuitafuta saini ya Guendouzi. Japokuwa, Arsenal mpango wao wa kubadilishana wachezaji bado upo palepale.Kwao (Arsenal) hii ndio njia pekee ya kuendana na madhara ya kiuchumi yaliyosababishwa na Mlipuko wa Virusi vya Corona duniani.

Arteta anamtizama Coutinho kama mchezaji mwenye faida zaidi kulingana na mfumo wake wa kiuchezaji. Anamtizama Coutinho kama mrithi wa Pierre-Emerick Aubameyang endapo mshambuliaji huyo ataamua kuondoka Emirate.

Pia, hali ya sintofahamu kuhusu hatma ya usajili wa Dani Ceballos anayechezea Arsenal kwa mkopo akitokea Real Madrid, inamuongezea mashaka Arteta katika nafasi hiyo. Endapo Ceballos ataamua kuondoka, Arteta atakosa mtu wa kuziba pengo hilo na hivyo Coutinho kuwa usajili wenye faida zaidi kwa Arsenal.

Arsenal watakuwa uwanjani leo kukipiga dhidi ya Chelsea katika fainali ya Kombe la FA. Ushindi kwa Arsenal ni faida kiuchumi, lakini pia itawapa tiketi ya moja kwa moja kushiriki michuano ya Europa msimu ujao.


Nini kinachokupa raha kama michezo ya kasino ya mtandaoni? Hasa unapojua kuwa kuna ushindi, jackpot na mizunguko kibao ya bure. Ungana na bwana Meridian kupata ushindi na burudani.

Cheza Hapa Sasa

44 Komentara

    Arteta anamtazama Countino Kama mchezaji mwenye faida

    Jibu

    Chelsea, arsenal, Tottenham wanatakiwa kujipanga kwenye pesa ndio atamchukua countinho

    Jibu

    Bonge la makala

    Jibu

    Coutinho kama atatua Arsenal itakuwa deal zuri sana kwa Arsenal anaweza wasaidia kuleta ushindani zaidi.

    Jibu

    Hitakua vizuri kama arsenal wakimsajili acountinho

    Jibu

    Jembe Hilo acontinho Arsenal msilaze damu kwa jembe hilo

    Jibu

    Continho Hana bahati kabisa ila ni mchezaji mahili Sana.

    Jibu

    bora coutinho angekuja zake arsenal arteta amuangalie kwa jicho la tatu

    Jibu

    Asante kwa makala nzuri #
    Meridianbettz

    Jibu

    Coutinho amekua hana bahati kabisa

    Jibu

    Coutinho nyota yake Kama imezimika tofauti na alivyokuwa akiwika mwanzo

    Jibu

    Kila lakheri kwa arsenal maana bado hawako vizuri .

    Jibu

    Countinho Kama atafanikiwah kwenda Arsenal ni sawa Kama kazima ndoto zake kuchukuwah mataj na kuchukuwah uchezaj Bora wa dunia vle

    Jibu

    Arsenal fanyen kwel msilaze damu!!!

    Jibu

    Makala yakijanjaa

    Jibu

    Maisha yanabadilika haraka sana Countinho kutoka kuwa nyota akiwa Liverpool hadi kutakiwa kuondoka ktk Klabu kwasababu ya kiwango duni#meridianbettz

    Jibu

    Arsenal bado kwa courtinho

    Jibu

    Coutinho yuko vizuri sana

    Jibu

    Coutinho yupo vizuri

    Jibu

    Itakuwa poa kama Coutinho ataenda arsenal hilo ni bonge la dili

    Jibu

    Asante kwa makala

    Jibu

    Me naona Bora asalie kwenye timu yake ya Sasa kuliko kwenda utopoloni# meridianbettz

    Jibu

    Bonge la makala#meridianbettz

    Jibu

    Makal nzur

    Jibu

    Hatari s

    Jibu

    Dili likikamilika la coutinho kwenda arsenal itakua vizuri sana

    Jibu

    Axante kwa taarifa nzur

    Jibu

    Habar njema

    Jibu

    Nic

    Jibu

    Good news

    Jibu

    Good news

    Jibu

    Nmefurahishwa na makala poa Sana.

    Jibu

    Asanteni meridianbet kwa makala nzuri

    Jibu

    Itakuwa vizuri akija arsenal

    Jibu

    Yuko vizuri kijana Arsenal wafanye kuweka dau kubwa mezani

    Jibu

    courtinho ni mchezaji mzuri la kuelekea arsenal mm naona ni Bure sana mana kuhama Liverpool ni sawa saw a na kiwango chako kimeshuka

    Jibu

    Ahsant sana meridianbet kwa taarifa

    Jibu

    Arsenal msilaze damuuu

    Jibu

    Arsenal wamchukue countino ni mchezaji mzuri Sana pia hataongeza nguvu katika kikosi pia countino hatarudi tena kukicheza katika ligi ya premier

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    History ilikuwa inaonyesha kabisa kuwa watamchukua kombe la FA

    Jibu

    Gud news

    Jibu

    I wish coutinho aende Arsenal atafanya meng mazur

    Jibu

    Habari nzuri sana

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.