Muelewe Vyema Mwamba Werner Usajili Konki wa Chelsea

Timo Werner anatarajia kuanza kupangwa kwenye kikosi cha The Blues baada ya kusajiliwa kwa dau la £45m akitokea klabu ya RB Leipzig msimu uliyopita.

Werner ni zao la akademi ya klabu ya Sturttgart, ana macho makali kama wembe katika goli.

STUTTGART, Timo Werner akisherehekea goli mwaka 2013

alikuwa kinara wa upachikaji magoli katika kikosi cha U-19 akiwa na umri wa miaka 16 aliweza kutupia wavuni mabao 24 na kuona akitunukiwa medali ya dhahabu ya Fritz Walter- Pia alipata tuzo ya kifahari ya mwaka nchini Ujerumani.

Alifanikiwa kuwa mchezaji mdogo wa Stuttgart anayecheza katika kikosi cha wakubwa na kufunga mabao mengi mwaka 2013-14 kabla hajasepa na kutua RB Leipzig mwezi Julai mwaka 2016.

Akiwa chini ya mwalimu kijana Julian Nagelsmann, Werner alipeleka soka lake katika levo nyingine.

Akisakata katika eneo la mshambuliaji wa kati alionesha umahairi wake kwa kufunga mabao 78 na kutoa asisti 32 katika ligi ya Bundesliga kwenye misimu minne iliyopita.

Timo Werner akiwa na umri wa miaka 24,amefungua ukurusa mpya wa maisha yake ya soka nchini Uingereza katika klabu ya Chelsea na jinsi anavyo jiamini anaonekana kasi yake ya kutingisha nyavu za wapinzani itaendelea.

Katika mahojiano yake ya kwanza na klabu, alisema “tumeongea sana na kocha [Lampard] kuhusu mfumo na namna ninavyoweza kucheza vyema.

“Anataka kunisaidia sio tuu kama mchezaji bali kibindamu na kufikia malengo yangu najisikia vizuri sana nina furaha kuwa hapa.

“Mtindo wa mpira wa Premier League ni wa kasi sana na mimi napenda mtindo huo nina kasi sana nadhani ni sehemu sahihi mimi kucheza.

Ingawa haijafahamika ni mtindo gani Chelsea itautumia kwa msimu mpya lakini Werner anaonekana kuweza kuendana na mtindo wowote pale iatapo hitajika. Werner atashirikiana vyema na wachezaji kama Tammy Abraham au Olivier Giroud

Mabeki wa vilabu mbali mbali vya Premier League watakuwa na kazi kubwa ya kuweza kumzuia mtaalamu Werner pindi wakitua Stamford Bridge.

Ukweli Kuhusu Timo Werner

Umri: 24                                                                                                                  Nafasi: Mshambuliaji
Utaifa: Ujerumani: (mechi 29, magoli 11)                                                                 Klabu ya sasa: Chelsea                                                                                          Vilabu alivyovichezea: RB Leipzig (michezo 159, magoli 95), Stuttgart (mechi 103, magoli 14)


Beti Mbio za Mbwa Mubashara

Hii ni rahisi zaidi! Hapa USHINDI unaupata kwa kuchagua mbwa anayeshinda mbio na machaguo mengine yenye odds tamu.

Cheza Hapa

42 Komentara

    Ni mchezaji mzuri sana toka akiwa rb amedhihirisha hilo lampard akimpatia walishaji wazuri basi hawatajutia usajili huu

    Jibu

    Record yake ni nzuri katika kupachika mabao atakua msaada mkubwa Sana darajani msimu ujao.

    Jibu

    Mchezaj mzuri anarekodi nzuri ngoj tuone darajan ataonyesh kitu gan hapo thnks meridian kwa update

    Jibu

    Ahsant meridian kwa taarifa

    Jibu

    Hapo Sasa Chelsea ndio wamefanya usajili wamemleta mchezaji anaejielewa

    Jibu

    Hongera Chelsea kwa kuleta jembe

    Jibu

    Ligi ya EPL ngumu, haijawahi kuwa rahisi kwa wachezaji kuzoea na kuwika tuone kama atawika Chelsea kama ilivyokuwa kwa Mjerumani mwenzie Michael Ballack#meridianbettz

    Jibu

    Aisee wametishaa

    Jibu

    Chelsea msimu naonwako vzur sana kweny usajil

    Jibu

    Ni kwer mchezaj mzur atawasaidia

    Jibu

    asante kwa update

    Jibu

    Yuko vizuri sana.

    Jibu

    Anarekodi nzuri sana katika soka Chelsea wakimpata itakua poa sana

    Jibu

    Ana rekodi nzuri hakika huyu ni mwamba km jina lake linasadifu, Chelsea kikosi chaxid kuimarik.

    Jibu

    Akaribie epl

    Jibu

    Yuko vizuri Sana

    Jibu

    Record yake ni nzuri katika kupachika mabao atakua msaada mkubwa Sana darajani msimu ujao.

    Jibu

    Big up Chelsea

    Jibu

    Maoni:karibu Chelsea

    Jibu

    Wametisha sana

    Jibu

    Wanajitaidi sana Chelsea kwa usajili huu hinawapa hamasa mashabiki wao..!

    Jibu

    Kijana ana history mzuri kwenye michezo

    Jibu

    Chelsea mko vizuri kwa usajili wenu

    Jibu

    Chelsea wako vizuri kwenye usajili
    @meridianbettz

    Jibu

    chelsea ni wakati wao sasa kusahihisha walipokosea na kujipanga upya

    Jibu

    Timo Werner ni mchezaji mzuri

    Jibu

    Yuko vzuri Sana

    Jibu

    Msimu huu Chelsea tuko vizuri sana tu nasubiri mchezo tu uwaze

    Jibu

    usajili konki wa chelsea

    Jibu

    EPL kuna changamoto Chelsea wasianze kutamba sana

    Jibu

    Good news

    Jibu

    Chelsea awamu itakayo kuja itakuwa Mambo mazuri mnasajili vifaa

    Jibu

    Wamelamba dume

    Jibu

    Hatutaki sifaa tuuu,tunataka kuona maajabu yake!!!

    Jibu

    Habari njema kwa mashabiki wa chelsea

    Jibu

    Nice

    Jibu

    Safi

    Jibu

    Hongera chelsea kwa kureta jembe#meridianbettz

    Jibu

    Pongezi kwao Chelsea

    Jibu

    Hongera Yake Sana

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.