Juma Kaseja Nitafanya kama Yule Mzee Alivyofanya Pale Stadio Olimpico

Katikati ya Simulizi ya Fransesco Totti wa watakatifu wa Roma liliingia jina la Juma Kaseja wa Kigoma. Huyu ni nyanda na yule kiungo. Huyu ni mmanyema tu wa pale Kasulu.


.
Wakati majonzi yakiendelea ndani ya Stadio Olimpico, kila mtu anasikitika ajuavyo. Nje ya uwanja lilikuja gari moja jekundu lenye chata za manispaa.
.
Mwanzoni hakuna aliyelijali sana, walijua tu hawa ni wasumbufu wa jiji wapo katika pilikapilika zao za kila siku. Labda wapo hapa kuhamisha kontena zao za bidhaa. Lakini haikuwa hivo. Leo walikuwa hapa kwa kazi tofauti
.
Alitokea mzee mmoja wa miaka kama sitini hivi, akashuka katika gari lake lililoongozana na hili la manispaa. Akapanda juu ya Tela na kudandia whinch iliyomnyanyua juu sana.
.
Ilimnyanyua juu sana, juu zaidi ya urefu wa kuta za Stadio Olimpico. Kisha akatulia zake kuangalia yanayoendelea ndani.

Stadio Olimpico

Akatazama mechi ikaisha, akatazama sherehe nzima ya kumuaga Totti, ilipomalizika na yeye akashuka na kudandia gari lake akaondoka zake.
.
Wakati wote watu waliacha shughuli zao wakimshangaa lakini yeye hakujali. Wengine walimuona kichaa lakini hakujali. Alichojali ni kuwa anamshuhudia shujaa wa Roma akimaliza kazi yake ndani ya Roma.


.
Alipanga kuingia uwanjani kama mashabiki wengine lakini alifika na kuambiwa tiketi zimeisha. Ndipo akakubali kuingia gharama ya kuwalipa manispaa ili tu auone mwisho wa Fransesco Totti. Pesa ni nini mbele ya heshima ya mtu aliyewatumikia kwa damu yake yote?
.
Baada ya kumshuhudia Juma Kaseja katikati ya milingoti kwa miaka mingi, ninasubiri siku atakayoamua kumaliza maisha yake na mpira. Nitakwenda kumuaga popote atakapokuwa.


.
Labda itakuwa kwa Mkapa, labda tutakuwa tunacheza dhidi ya Misri ya Mohamed Salah. Labda uwanja utakuwa umejaa na nitakosa tiketi. Nitafanya nini??


.
Nitageuka yule mzee wa Italia, nionekane kichaa na watu lakini nimuage Juma Kaseja baada ya safari yake ndefu.
.
Baada ya Siku hiyo nitasubiri siku moja niwasimulie wajukuu zangu mechi zake bora kuwahi kutokea. Kuanzia kwa Zamalek pale Misri, mpaka CECAFA pale Uganda. NITASUBIRI


VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!

Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini???

SOMA ZAIDI

13 Komentara

    Kaseja alikua zamani

    Jibu

    Nakuwerewa mzee wakaz ukoseagi kaseja

    Jibu

    K juma kipa makin

    Jibu

    Habari nzuri sana

    Jibu

    Nice

    Jibu

    Zamani sio sasa Hana jipya

    Jibu

    Zamani alikuwa anatamba sio sasa

    Jibu

    Hana jipya juma kaseja

    Jibu

    Maneno nimeyaelewa

    Jibu

    Nyota ya kaseja imeshuka asikiki tena kama zamani

    Jibu

    Kaseja alikuwa vizuri zamani saiz hasikiki hata

    Jibu

    Ni ww tu

    Jibu

    Goodnews

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.