Lionel Messi atakosa mchezo wa Barcelona na Eibar siku ya Jumanne baada ya kupewa mapumziko zaidi ya Krismasi.

Nahodha huyo wa Barcelona yeye na familia yake walikwenda Rosario kwa kipindi cha sikukuu na hatarajiwi kurudi Catalonia hadi mwaka mpya, kabla ya mechi ya LaLiga dhidi ya Huesca mwezi Januari 3.
Barca ilirudi mazoezini siku ya Jumapili baada ya kupewa likizo ya siku nne kufuatia ushindi wa 3-0 dhidi ya Real Valladolid.
Klabu hiyo ilithibitisha Messi anatarajiwa kurudi katika vituo vya Camp Tito Vilanova baada ya mkutano wa ligi na vijana wa Jose Luis Mendilibar katika dimba la Camp Nou.
Kulingana na Sport, kocha mkuu Ronald Koeman alimpatia Messi ruhusa ya kukaa kwa muda mrefu nchini Argentina kwani anaonekana kumuweka mshindi mara sita wa Ballon d’Or akiwa fiti kabisa.
Baada ya kuanza kwa msimu mgumu kufuatia jaribio lake la kutaka kuondoka klabuni, Messi amepata fomu, akifunga mabao sita kati ya saba ya ligi mwaka 2020-21 katika mechi zake nane za hivi karibuni.
Barca wako nafasi ya tano katika LaLiga, alama nane nyuma ya vinara Atletico Madrid, wakiwa wamecheza mchezo zaidi.
VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!
Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini???



Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri Sana mwamba messi
warda
Hadi raha akirudi arudi na nguvu mpya
Rahmal
Safi sana messi
Adelta
Messi Yuko makini mashabiki wanamkubali sana
Shakila mrope
Hongera zako messi raha jipe mwenyewe
Sarah
Messi akirudi anarudi nanguvu mpya
Chiku
Mesi anajua anachokifanya hana shoo mbovu
Tatu
Bora ajitulizie na family yake
Mwanahamisi
Safi
Dorophina
Bora amepata mda wa kupumzika akirudi anarudi na Kasi mpya
Hopemwaikuka
Enjoy Messi
Angelina
Kwa raha zake