Baada ya mabosi wa Yanga kumtambulisha rasmi mrithi wa mikoba ya Cedric Kaze kwa mashabiki wao tayari ameanza kazi kwa ajili ya kukinoa kikosi hicho kuelekea kwenye mechi za Ligi Kuu Bara pamoja na Kombe la Shirikisho.
Nasreddine Nabi ambaye ni raia wa Tunissia amepewa dili la mwaka mmoja na nusu kukinoa kikosi hicho ambacho kilikuwa mikononi mwa Juma Mwambusi aliyekuwa akikaimu nafasi ya Kaze iliyoachwa wazi tangu Machi 7, 2021.

Raia huyo wa Tunissia jana alianza kuwanoa nyota wa kikosi hicho wakiongozwa na kipa Faroukh Shikhalo, Ditram Nchimbi, Kibwana Shomari, Feisal Salum, Saido Ntibanzokiza kwa ajili ya mechi ya kesho ya ligi dhidi ya Azam FC.
Yanga ikiwa inaongoza ligi baada ya kucheza mechi 26 kesho Uwanja wa Mkapa inakazi ya kusaka pointi tatu mbele ya Azam FC kwenye mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.

Azam ipo nafasi ya tatu na pointi 51 inakutana na vinara wenye pointi 57 jambo ambalo litaongeza ushindani.
Kwenye mchezo wa kwanza walipokutana Uwanja wa Azam Complex, ubao ulisoma Azam 0-1 Yanga.
Nabi amesema kuwa anatambua wachezaji wake wapo imara na amewaambia kwamba wana kazi ya kuonyesha vitendo kwenye mechi zote.
Nafasi nyingine kwaajili yako, kasino mpya yenye hadhi ya kipekee inayokupa kila sababu ya kuwa mshindi katika kasino za Meridianbet, anza siku yako na njia rahisi ya kutengeneza mkwanja.



Sarah
Tunasubiri tuone maajabu yake
Adelta
Vizuri kabisaa sisi mashabiki tunasubiri tuone matokeo mazuri
aisha
Kila la kher
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri kila la kheri kwake
Magdalena
Kila la kheri kwake
Khadija
Tunasubili tuone
Issa
Wape salam
Johnmary jo
Hongera kwa klabu ya yanga#meridianbett#
warda
Kweli ameanza
Furahav
Hongera kwake.