YANGA: Kocha Mpya Ameanza Kazi Rasmi

Baada ya mabosi wa Yanga kumtambulisha rasmi mrithi wa mikoba ya Cedric Kaze kwa mashabiki wao tayari ameanza kazi kwa ajili ya kukinoa kikosi hicho kuelekea kwenye mechi za Ligi Kuu Bara pamoja na Kombe la Shirikisho.

Nasreddine Nabi ambaye ni raia wa Tunissia amepewa dili la mwaka mmoja na nusu kukinoa kikosi hicho ambacho kilikuwa mikononi mwa Juma Mwambusi aliyekuwa akikaimu nafasi ya Kaze iliyoachwa wazi tangu Machi 7, 2021.

Yanga - Nabi conference

Raia huyo wa Tunissia jana alianza kuwanoa nyota wa kikosi hicho wakiongozwa na kipa Faroukh Shikhalo, Ditram Nchimbi, Kibwana Shomari, Feisal Salum, Saido Ntibanzokiza kwa ajili ya mechi ya kesho ya ligi dhidi ya Azam FC.

Yanga ikiwa inaongoza ligi baada ya kucheza mechi 26 kesho Uwanja wa Mkapa inakazi ya kusaka pointi tatu mbele ya Azam FC kwenye mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.

Yanga - Talking

Azam ipo nafasi ya tatu na pointi 51 inakutana na vinara wenye pointi 57 jambo ambalo litaongeza ushindani.

Kwenye mchezo wa kwanza walipokutana Uwanja wa Azam Complex, ubao ulisoma Azam 0-1 Yanga.

Nabi amesema kuwa anatambua wachezaji wake wapo imara na amewaambia kwamba wana kazi ya kuonyesha vitendo kwenye mechi zote.


MKWANJA MARIDHAWA NA KASINO YA 777 MEGA DELUXE

Nafasi nyingine kwaajili yako, kasino mpya yenye hadhi ya kipekee inayokupa kila sababu ya kuwa mshindi katika kasino za Meridianbet, anza siku yako na njia rahisi ya kutengeneza mkwanja.

CHEZA HAPA

10 Komentara

    Tunasubiri tuone maajabu yake

    Jibu

    Vizuri kabisaa sisi mashabiki tunasubiri tuone matokeo mazuri

    Jibu

    Kila la kher

    Jibu

    Vizuri kila la kheri kwake

    Jibu

    Kila la kheri kwake

    Jibu

    Tunasubili tuone

    Jibu

    Wape salam

    Jibu

    Hongera kwa klabu ya yanga#meridianbett#

    Jibu

    Kweli ameanza

    Jibu

    Hongera kwake.

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.