Carlos Sainz anasema kuwa mwanatimu mwenzake Lando Norris anastahili mkataba wake mpya uliotangazwa na McLaren kutokana na mchango wake mkubwa katika timu.
Mwaka jana na mwaka 2019, madereva hawa walikuwa wanawekwa pamoja na kufananishwa sana pale McLaren, huku Sainz akipokea ofa ya kuungana na Ferrari kwa mwaka 2021.
McLaren sasa wametangaza nyongeza ya mkataba wa kinda huyu wa miaka 21. Norris ataendelea kuwepo hapo kwa miaka miwili zaidi, na kwa mujibu wa Sainz mwanatimu mwenzake anastahili kabisa ofa hii.
“Kuna kundi kubwa la madereva ambao wanapambania viwango kama hivyo, na ninaweza kumjumuisha Lando miongoni mwao.” – Sainz
“Wote ni mabingwa watarajiwa, na wanahitaji gari sahihi tu kuweza kuchukua taji.” akijijumuisha yeye na mwanatimu mwenzake Charles Leclerc.
Sainz anaamini kuwa Norris anauwezo mkubwa wa kuisaidia McLaren, japokuwa Formula 1 inategemea zaidi namna timu inavyofanya kuliko mchezaji mwenyewe.
Zungusha na ushinde mkwanja wako papo hapo baada ya mzunguko kukamilika. Ni kugusa tu 🤑.
Shakila
Nice update